Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waefeso 6:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 “Kusudi upate heri na uishi siku nyingi katika dunia.”

Gade chapit la Kopi




Waefeso 6:3
15 Referans Kwoze  

“Uheshimu baba yako na mama yako, kama vile mimi Yawe, Mungu wako, nilivyokuamuru, kusudi uishi maisha marefu na kufanikiwa katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Kwa hiyo mushike masharti yake na amri zake ambazo ninawapa leo kusudi mufanikiwe, ninyi pamoja na wazao wenu, na kuishi siku nyingi katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa ikuwe yenu milele.”


Mufanye angalisho kutii maneno haya niliyowaamuru, kusudi mupate kufanikiwa ninyi pamoja na wazao wenu nyuma yenu milele, maana mutakuwa munatenda mazuri na kwa usawa mbele ya Yawe, Mungu wenu.


Musikule damu, nanyi mutafanikiwa pamoja na wazao wenu, maana mutakuwa munatenda kwa usawa mbele ya Yawe.


Kwa hiyo enyi Waisraeli, mukuwe waangalifu kwa kuzitimiza, kusudi mufanikiwe na kuongezeka sana katika inchi hiyo inayotiririka maziwa na asali kama vile alivyowaahidi.


Utamwacha mama ndege aende zake, lakini unaweza kutwaa vitoto. Ukifanya hivyo utafanikiwa na kuishi maisha marefu.


Ikuwe ni jambo la kupendeza au hapana, sisi tutaitii sauti ya Yawe, Mungu wetu, ambaye tunakutuma kwake kusudi mambo yatuendekee vizuri tutakapomutii Yawe, Mungu wetu.


Muwaambie watu wa haki jinsi wanavyokuwa na heri, maana watakula matunda ya matendo yao.


Siku moja, Naomi mama mukwe wa Ruta akamwambia: “Inanipasa kwangu kukutafutia mume kusudi upate uheri.


Mufanye yale yanayomupendeza Yawe, kusudi mupate kufanikiwa. Mutaweza kuirizi inchi ile nzuri ambayo Yawe aliapa kuwapa babu zenu,


Mutafuata njia yote Yawe, Mungu wenu, aliyowaamuru kufuata kusudi mambo yenu yawaendekee vizuri na mupate kuishi muda murefu katika inchi mutakayotwaa ikuwe mali yenu.


Musijenge nyumba, musilime mashamba, wala musikuwe na shamba la mizabibu. Lakini mutaishi katika mahema siku zote za maisha yenu, kusudi mupate kuishi siku nyingi katika inchi munamoishi kama wageni.


“Heshimu baba yako na mama yako.” Hii ni amri ya kwanza ambayo waliongeza ahadi hii juu yake:


Na ninyi wababa musiwakasirikishe watoto wenu. Lakini muwalee na kuwaonya, mukiwatolea mashauri yanayotoka kwa Bwana.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite