Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waefeso 4:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Basi, neno hili “alipanda juu,” lina maana gani? Maana yake ni kusema kwamba alishuka kwanza mpaka chini katika dunia.

Gade chapit la Kopi




Waefeso 4:9
22 Referans Kwoze  

Na zaidi ya hii hakuna mutu aliyepanda mbinguni, isipokuwa Mwana wa Mutu aliyeshuka toka mbinguni.


Kwa maana, kama vile Yona alivyobaki ndani ya tumbo la samaki mukubwa kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku, ndivyo vilevile Mwana wa Mutu atakavyobaki ndani ya udongo kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.


Maana mukate Mungu anaoupana ni yule anayeshuka toka mbinguni na kuleta uzima katika dunia.”


Ni nani aliyepanda juu mbinguni na kushuka chini? Ni nani aliyekamata upepo katika mukono? Ni nani aliyefunga maji katika kitambaa? Ni nani aliyeweka mipaka yote ya dunia? Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwana wake? Uniambie kama unajua!


Roho yangu inashikamana nawe kabisa; unanilinda kwa mukono wako wa kuume.


Lakini mambo tunayoona ndiyo haya: Yesu alifanywa kuwa mwenye cheo chini kidogo ya malaika kusudi kwa neema ya Mungu, Yesu akufe kwa ajili ya watu wote. Na sasa kwa njia ya kile kifo kilichomufikia, amepata utukufu na heshima.


Yesu akamwambia: “Usinishike, kwa sababu sijapanda bado kwa Baba. Lakini kwenda kwa wandugu zangu na kuwaambia kwamba ninapanda kwa Baba yangu anayekuwa Baba yenu vilevile, anayekuwa Mungu wangu na Mungu wenu vilevile.”


mutu ni nini, ee Mungu, hata umufikirie? Mwanadamu ni nini hata umujali?


Halafu Yawe akashuka chini kuona muji ule na munara ambayo wanadamu walijenga.


Umemufanya kuwa mwenye cheo chini kidogo ya malaika. Umemujaza utukufu na heshima.


Yesu akawajibu: “Hata nikijishuhudia mimi mwenyewe, ushuhuda wangu ni wa kweli, kwa sababu ninajua pahali nilipotoka na pahali ninapokwenda. Lakini ninyi hamujui pahali nilipotoka wala pahali ninapokwenda.


Basi itakuwa namna gani kama mukimwona Mwana wa Mutu akipanda tena pahali alipokuwa mbele?


Huu ndio mukate ulioshuka toka mbinguni, nao si kama mukate ule babu zenu waliokula katika jangwa na kufa. Anayekula mukate huu ataishi milele.”


Mimi ni ule mukate wa uzima, ulioshuka toka mbinguni. Kama mutu akikula mukate huu ataishi milele. Na mukate nitakaotoa ni mwili wangu, utakaotolewa kusudi dunia ipate uzima.”


Basi Wayuda wakaanza kunungunika kwa sababu Yesu alisema kwamba yeye ni mukate ulioshuka toka mbinguni.


Kwa sababu nimeshuka toka mbinguni kusudi nifanye mapenzi ya yule aliyenituma, wala si mapenzi yangu.


Muimbe kwa furaha enyi mbingu, kwa sababu ya yale Yawe aliyotenda. Mupige kelele enyi vilindi vya dunia! Mupige vigelegele enyi milima! Enyi mapori na miti yote inayokuwa ndani yake, mushangilie. Maana Yawe amewakomboa wazao wa Yakobo, naye atatukuzwa katika inchi ya Israeli.


Umbo langu halikufichikwa kwako nilipoumbwa kwa uficho, nilipotengenezwa ndani ya tumbo la mama yangu.


Yawe akashuka juu ya mulima Sinai, akamwita Musa kutoka kule juu, naye Musa akapanda juu ya mulima.


Hayo yameupata kusudi muti wowote unaokuwa pahali penye maji usiweze kurefuka tena kwa kimo hicho wala kukifikisha kilele chake katika mawingu. Muti wowote unaokunyweshwa maji usiweze tena kufikia urefu huo. Kwa maana kila kitu mwisho wake ni kifo; hata na watu vilevile. Wote watashiriki hali ya wanaoshuka katika shimo kwa wafu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite