Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waefeso 4:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Mungu mumoja, Baba ya watu wote, anayekuwa juu ya wote, anayetumika kwa njia ya wote, na anayekaa ndani ya wote.

Gade chapit la Kopi




Waefeso 4:6
31 Referans Kwoze  

Kwa maana vitu vyote vinatoka kwake, navyo viko kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Atukuzwe hata milele! Amina.


Ingawa hivi, kwa ngambo yetu sisi tuko na Mungu mumoja peke yake tu, ndiye Baba aliyeumba vitu vyote, nasi tunaishi kwa nguvu yake. Vilevile kuko Bwana mumoja tu, ndiye Yesu Kristo. Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, nasi tunaishi kwa nguvu yake.


Sisi wote si watoto wa baba mumoja? Sisi wote hatukuumbwa na Mungu yuleyule? Mbona basi, hatuaminiani sisi kwa sisi, na tunalizarau agano Yawe alilofanya na babu zetu?


Yesu akamwambia: “Usinishike, kwa sababu sijapanda bado kwa Baba. Lakini kwenda kwa wandugu zangu na kuwaambia kwamba ninapanda kwa Baba yangu anayekuwa Baba yenu vilevile, anayekuwa Mungu wangu na Mungu wenu vilevile.”


Mutu anayetii amri za Mungu anakaa ndani yake, na Mungu anakaa ndani ya yule mutu. Tunatambua kwamba Mungu anakaa ndani yetu kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetupatia.


Basi muangalie namna munavyopaswa kusema munapoomba: ‘Baba yetu unayekuwa mbinguni, Jina lako litukuzwe;


Kuna ulinganisho gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi ni hekalu la Mungu Mwenye Uzima kama vile yeye mwenyewe alivyosema: “Nitakaa na kuishi pamoja nao, nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”


Kuna kazi za namna mbalimbali, lakini Mungu ni mumoja anayewezesha watu wote kuzitimiza.


Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?


akamubariki Abramu akisema: “Abramu abarikiwe na Mungu Mukubwa, Muumba wa mbingu na dunia!


Ninawatakia wandugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kwa Bwana Yesu Kristo.


Hivi Kristo apate kukaa ndani ya mioyo yenu kwa njia ya imani, nanyi mupate kuwa na mizizi na musingi katika upendo.


Katika kuungana pamoja na Kristo, ninyi vilevile munaunganishwa pamoja na wengine wote kuwa makao ya Mungu kwa njia ya Roho wake.


Nimekujulisha kwao, na nitaendelea kukujulisha kusudi upendo ule unaokuwa nao kwangu ukuwe ndani yao, nami mwenyewe nikuwe ndani yao.”


Yesu akamujibu: “Anayenipenda, atashika maneno yangu. Baba yangu atamupenda, naye Baba pamoja nami tutaingia ndani yake na kukaa ndani yake.


Usituache kuanguka katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. [Kwa maana ufalme, uwezo na utukufu ni vyako hata milele. Amina.]’


Maana wewe ndiwe Baba yetu; Abrahamu, babu yetu, hatujali, naye Israeli hatutambui; lakini wewe, ee Yawe, ni Baba yetu. Wewe umeitwa tangu zamani: Mukombozi wetu.


Maana Yawe ni Mungu mukubwa; yeye ni mufalme mukubwa juu ya miungu yote.


Na kule anatawala juu ya wakubwa wote, wenye mamlaka wote, wenye uwezo wote na wasultani wote na juu ya kila cheo kinachoweza kuwa katika dunia hii na katika dunia itakayokuja.


“Basi musikilize, enyi Waisraeli! Yawe, Yawe tu, ni Mungu wetu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite