Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waefeso 3:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Hakika, mumesikia jinsi Mungu alivyonijalia neema, akinipatia kazi ya kufanya kwa ajili yenu.

Gade chapit la Kopi




Waefeso 3:2
27 Referans Kwoze  

Mafundisho haya yanalingana na Habari Njema ya utukufu wa Mungu mwenye baraka, ambayo nilipewa nipate kuihuburi.


Kwa ajili ya Habari Njema hii, nimewekwa kuwa mujumbe, mutume na mwalimu,


Kwa njia yake Mungu amenipa neema ya kuwa mutume kusudi niongoze mataifa yote yapate kumwamini na kumutii. Na kwa tendo hilo jina lake lipate kusifiwa.


Lakini kila mutu kati yetu alipokea neema kadiri ya kipimo alichojaliwa na Kristo.


Kwa hiyo mutuhesabu kama watumishi wa Kristo, wanaoshugulika na ujumbe wa siri wa Mungu.


Kusudi la mupango ule utakaotimia kwa wakati uliowekwa, ni kukusanya viumbe vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia chini ya utawala wa Kristo.


Mumesikia namna mwenendo wangu ulivyokuwa zamani, wakati nilipofuata dini ya Kiyuda. Munajua namna nilivyotesa kanisa la Mungu vikali sana na kujikaza kwa kuliharibu.


Halafu Bwana akaniambia: ‘Kwenda, kwa maana nitakutuma mbali kwa watu wa mataifa mengine.’ ”


Halafu Paulo na Barnaba wakawaambia bila woga: “Ilitupasa kwanza kuhubiri Neno la Mungu kwenu. Lakini kwa kuona mumelikataa na kujihesabu ninyi wenyewe kwamba uzima wa milele haufai kwenu, basi tunashugulika na watu wa mataifa mengine.


Siku moja walipokuwa wakifanya ibada, wakiwa wamefunga kula chakula, Roho Mutakatifu akasema: “Muwasimike Barnaba na Saulo kwa kazi ile niliyowachagulia.”


Lakini Bwana akamwambia: “Kwenda tu, kwa maana nimemuchagua mutu huyu kwa kunitumikia, kusudi atangaze jina langu kwa mataifa, kwa wafalme na kwa Waisraeli.


Ni kwa hiyo nimewekwa kuwa mujumbe na mutume kwa kuwafundisha watu wa mataifa mengine kusudi wapate kumwamini Mungu na kutambua ukweli. Mimi ninasema ukweli wala si uongo.


Uwaambie wasishikamane na hadisi za uongo, pamoja na mambo yasiyokuwa na mwisho ya wababu. Hayo yote yanaleta mabishano, wala hayafai kitu kwa kutimiza mupango wa Mungu wa wokovu, unaojulikana kwa njia ya imani.


Habari Njema ile inatoa matunda na kuenea katika dunia yote sawa vile ilivyofanya kwenu tangu siku ile muliposikia wakisema juu ya neema ya Mungu na kupata kuitambua inavyokuwa kweli.


Hayo yote ni kwa maana tumesikia namna munavyomwamini Yesu Kristo na namna munavyowapenda watu wote wa Mungu.


Hakika mumesikia habari zake, nanyi mukiwa waamini mumefundishwa kufuatana na ukweli unaokuwa ndani ya Kristo.


Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.


Kufuatana na neema niliyopewa na Mungu, ninawaambia ninyi wote: mutu asijiwazie kuwa na ukubwa kupita vile inavyomustahili. Lakini mukuwe na mawazo ya ukadirifu, kila mumoja kulingana na kipimo cha imani aliyopewa na Mungu.


Sasa ninasema na ninyi watu wa mataifa mengine. Nami ninafurahia kazi yangu, kwa kuona nimetumwa kuwa muhubiri wa watu wa mataifa.


Nimewekwa kuwa mutumishi wa Habari Njema kwa njia ya zawadi Mungu aliyonipatia kutokana na uwezo wake.


Na hivi nipate kuwaelezea vema namna unavyotimia ule mupango uliokuwa umefichwa tangu zamani na Mungu, muumbaji wa vitu vyote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite