Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waefeso 3:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Lakini sasa, kwa njia ya kanisa, watawala na wote wenye uwezo wanaokuwa katika eneo la mbingu wapate kutambua hekima ya Mungu inayokuwa ya namna nyingi.

Gade chapit la Kopi




Waefeso 3:10
23 Referans Kwoze  

Mungu aliwafunulia wale manabii kwamba ujumbe ule walioutangaza haukuwaelekea wao wenyewe, lakini uliwaelekea ninyi. Na sasa ujumbe ule umetangazwa kwenu na wale waliowahubiri Habari Njema kwa uwezo wa Roho Mutakatifu aliyetumwa toka mbinguni. Hata wamalaika vilevile wanatamani kujua mambo hayo.


Kwa maana hatupigani na watu wa dunia hii, lakini tunapigana na pepo mbaya zinazokaa katika eneo la mbingu pamoja na wakubwa, na wenye mamlaka na watawala wa dunia hii ya giza.


Ninatangaza hekima ya siri ya Mungu, hekima iliyofichwa kwa watu, na iliyopangwa na Mungu mbele ya kuumbwa kwa dunia kwa ajili ya utukufu wetu.


Utajiri wa Mungu, hekima na ufahamu wake ni vikubwa kupita kipimo! Hakuna anayeweza kuvumbua kusudi lake wala kuelewa mipango yake!


Na kule anatawala juu ya wakubwa wote, wenye mamlaka wote, wenye uwezo wote na wasultani wote na juu ya kila cheo kinachoweza kuwa katika dunia hii na katika dunia itakayokuja.


Asifiwe Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Yeye ndiye aliyetupatia baraka za kiroho za kila namna kutoka katika eneo la mbingu kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo.


Lakini kwa wale walioitwa na Mungu, ikiwa Wayuda au wasiokuwa Wayuda, Kristo ni kitambulisho cha uwezo na hekima ya Mungu.


aliyepanda mbinguni, na anayekaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu, akitawala wamalaika, nao wenye mamlaka na uwezo wanaokuwa katika mbingu.


Kwa njia yake, Mungu aliumba vitu vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia, vyenye kuonekana na visivyoonekana; ikiwa ni ufalme, ukubwa, utawala au mamlaka. Mungu aliumba vyote kwa njia yake na kwa ajili yake.


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


akitupatia hekima na akili kamili.


Kwa maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kinachoweza kututenga na upendo wa Mungu: wala kifo, wala uzima, wala wamalaika, wala watawala, wala mambo ya sasa, wala mambo yatakayokuja, wala wenye uwezo,


Ee Yawe, matendo yako ni mengi sana! Umeyafanya kwa hekima yote! Dunia imejaa viumbe vyako!


Kisha Roho akaninyanyua juu, nami nikasikia nyuma yangu sauti kama ya tetemeko kubwa ikisema: Utukufu wa Yawe usifiwe mbinguni.


Mumusifu Yawe, enyi wamalaika wakubwa, enyi munaotimiza amri zake na kutimiza neno lake!


Kanisa ni mwili wa Kristo, nalo ni utimilifu wa Kristo anayetimiza vitu vyote.


Na kwa kuungana naye, ninyi mumepata kukamilika. Yeye ndiye anayetawala roho zote zenye mamlaka na uwezo.


Mungu alinyanganya uwezo wa wakubwa na wenye mamlaka, naye akawaonyesha waziwazi, akiwatembeza kama wafungwa katika maandamano ya ushindi wa Mwana wake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite