Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waefeso 2:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 sisi tuliokuwa tumekufa kwa sababu ya makosa yetu, alitufufua pamoja na Kristo. Hivi mumeokolewa kwa neema ya Mungu.

Gade chapit la Kopi




Waefeso 2:5
20 Referans Kwoze  

Lakini kwa neema ya Mungu wanahesabiwa haki kwa bure kwa njia ya Kristo Yesu anayewakomboa.


Kwa maana mumeokolewa kwa neema ya Mungu, kwa njia ya imani. Jambo hili halitokani na ninyi wenyewe, lakini ni zawadi ya Mungu.


Basi ikiwa kama tulipokuwa waadui za Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kufa kwa Mwana wake, inaonyesha zaidi sana kwamba tukiwa tumepatanishwa naye, tutaokolewa kwa njia ya uzima wa Kristo.


Lakini Mungu ameonyesha wazi upendo wake kwetu ni wapata gani, kwa maana tulipokuwa tungali wenye zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.


Haipaswi kuwa vile, kwa maana sisi na wao vilevile tunaamini kwamba sisi wote tunaokolewa kwa neema ya Bwana Yesu.”


Zamani ninyi mulikuwa mumekufa kiroho kwa sababu ya makosa na zambi zenu.


Maana sheria ya Roho anayepana uzima kwa kuungana na Yesu Kristo imetuweka kuwa huru kutoka sheria ya zambi na ya kifo.


Kwa maana neema ya Mungu inayoleta wokovu kwa watu wote imeonekana waziwazi.


Kwa maana yote yanayoonekana wazi yanageuka mwangaza. Ni kwa hiyo inasemwa hivi: “Amuka wewe unayelala! Ufufuke kutoka kati ya wafu, naye Kristo atakuangazia.”


Kwa hiyo ahadi inafuatana na imani, kusudi ikuwe imetolewa kwa neema ya Mungu. Na zaidi kuwe uhakikisho kwamba ahadi hiyo ni kwa ajili ya wazao wote wa Abrahamu, si kwa wale wanaotii Sheria tu, lakini vilevile kwa wale wanaokuwa na imani kama Abrahamu, babu yetu sisi wote.


alituokoa sisi. Hakufanya vile kwa sababu ya matendo yetu ya haki, lakini alituokoa kwa sababu ya huruma yake kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetuwezesha kuzaliwa mara ya pili na kuwa na maisha mapya kwa kutusafisha kwa maji.


Kwa maana tulipokuwa hatuna uwezo wowote, Kristo alikufa kwa ajili ya waovu kwa wakati uliopangwa.


Mungu, anayeleta amani, atamupondaponda sasa hivi Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo ikuwe pamoja nanyi.


Roho ndiye anayeleta uzima; mwili hauwezi kufaa kitu. Maneno haya niliyosema nanyi, ndiyo Roho na uzima.


Kwa maana kama vile Baba anavyofufua wafu na kuwarudishia uzima, vile vile Mwana anawapa uzima wale anaowataka.


Ninawatakia ninyi wote neema kutoka kwa Bwana Yesu. Amina.


Kwa sababu mwana wangu huyu alikuwa amekufa, na amefufuka, alikuwa amepotea na sasa ameonekana.’ Nao wakaanza kufurahi pamoja.


Zamani mulikuwa mumekufa kwa sababu ya zambi zenu na kwa sababu mulikuwa watu wa mataifa mengine, wasiotahiriwa. Lakini sasa, Mungu amewapatia ninyi uzima pamoja na Kristo, naye ametusamehe zambi zetu zote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite