Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waefeso 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Asifiwe Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Yeye ndiye aliyetupatia baraka za kiroho za kila namna kutoka katika eneo la mbingu kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo.

Gade chapit la Kopi




Waefeso 1:3
39 Referans Kwoze  

Tumusifu Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kubwa ametupatia uzima mupya kwa njia ya kumufufua Yesu Kristo. Na kwa hiyo tumepata tumaini lenye uzima,


Asifiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mwenye kujaa huruma na Mungu anayefariji katika mambo yote!


Katika kuungana kwetu na Yesu Kristo, Mungu ametufufua pamoja naye kusudi tutawale pamoja naye mbinguni.


Kutokana na wazao wako mataifa yote katika dunia yatabarikiwa kwa sababu wewe umeitii amri yangu.”


Alifanya vile wakati alipomufufua Kristo na kumwikalisha na mamlaka kwa kuume kwake mbinguni.


Jina lake tukufu litukuzwe milele; utukufu wake ujae katika ulimwengu wote! Amina, Amina!


Kwa maana hatupigani na watu wa dunia hii, lakini tunapigana na pepo mbaya zinazokaa katika eneo la mbingu pamoja na wakubwa, na wenye mamlaka na watawala wa dunia hii ya giza.


Lakini sasa, kwa njia ya kanisa, watawala na wote wenye uwezo wanaokuwa katika eneo la mbingu wapate kutambua hekima ya Mungu inayokuwa ya namna nyingi.


Kufuatana na hiyo, Mungu atawabariki wote wanaoamini sawa vile alivyomubariki Abrahamu, mwenye imani.


Lakini Yebesi alimwomba Mungu wa Israeli akisema: “Ee Mungu, ninakusihi unibariki na kupanua mipaka yangu. Mukono wako ukuwe pamoja nami na unilinde kutokana na jambo lolote ovu, na mateso yasinipate.” Naye Mungu akamupa yale aliyoomba.


Wazao wao watajulikana kati ya mataifa; watajulikana kati ya watu wengine. Kila mutu atakayewaona atakubali kwamba wao ni watu waliobarikiwa na Yawe.


Yawe akubariki kutoka Sayuni; yeye aliyeumba mbingu na dunia.


Ninaomba kusudi wote wakuwe mumoja, kama vile wewe Baba unavyokuwa ndani yangu na mimi ndani yako. Ninaomba vilevile kwamba wakuwe ndani yetu, kusudi dunia ipate kuamini kwamba umenituma.


Jina la mufalme litukuzwe siku zote; utukufu wake udumu muda wote jua litakapokuwa. Kwake mataifa yote yabarikiwe; watu wote wamwite mwenye heri!


Kisha, mufalme Daudi akawaambia wote waliokusanyika: “Mumusifu Yawe, Mungu wenu.” Na wote waliokusanyika wakamutukuza Yawe, Mungu wa babu zao, wakainama mbele yake na kumwabudu Yawe na kumutolea mufalme Daudi heshima.


Ninamwomba Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mwenye utukufu, awapatie Roho wake kusudi mukuwe na hekima na ufunuo hata muweze kumujua.


Mungu Baba ya Bwana Yesu, anayetukuzwa hata milele, anajua kwamba sisemi uongo.


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Atukuzwe Mungu Mukubwa, aliyetia waadui zako katika mikono yako!” Naye Abramu akamupa Melkisedeki sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo.


Kwa maana, Kristo ni kama mwili mumoja unaokuwa na viungo vingi. Ijapokuwa viungo vya mwili ni vingi, vinakuwa mwili mumoja tu.


Hivi vilevile, sisi tunaokuwa wengi tumekuwa mwili mumoja katika kuungana kwetu na Kristo, na sisi wote ni viungo kila mumoja kwa mwingine.


Na sasa, mimi Nebukadneza ninamusifu na kumutukuza na kumuheshimu Mufalme wa mbinguni. Maana matendo yake yote ni ya haki, naye anawashusha wenye kiburi.


Kusudi la mupango ule utakaotimia kwa wakati uliowekwa, ni kukusanya viumbe vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia chini ya utawala wa Kristo.


Basi mutu yeyote anapoungana na Kristo, yeye anakuwa kiumbe kipya. Mambo ya zamani yametoweka, na sasa hali mupya imefika.


Hivi kusudi mutaweza kwa nia moja na kwa sauti moja kumutukuza Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo.


Walawi, ni kusema Yesua, Kadimieli, Bani, Hasabuea, Serebia, Hodia, Sebania na Petahia, wakawaambia watu: Musimame na kumusifu Yawe, Mungu wenu. Mumusifu milele na milele! Na watu wakasifu jina lako tukufu, ambalo linatukuka kuliko baraka na sifa zote.


Kazi wale makuhani wanayofanya ni mufano na kitambulisho kinachoonyesha jinsi mambo kamili yanavyopitika mbinguni. Maneno hayo yanalingana na yale yaliyomutokea Musa. Wakati Musa alipokuwa karibu ya kujenga Hema, Mungu alimwambia: “Ufanye angalisho kusudi upate kutengeneza kila kitu kufuatana na mufano niliokuonyesha kwa mulima.”


na kila mutu akubali kwamba Yesu ni Bwana, naye Mungu Baba atatukuzwa kwa njia hiyo.


Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.


Basi ilikuwa lazima vitu vile vinavyoonyesha mufano wa mambo yanayopitika katika mbingu vitakaswe kwa njia ile. Lakini mambo kamili ya mbinguni yanahitaji kutakaswa kwa sadaka inayokuwa bora zaidi.


Yesu akamwambia: “Usinishike, kwa sababu sijapanda bado kwa Baba. Lakini kwenda kwa wandugu zangu na kuwaambia kwamba ninapanda kwa Baba yangu anayekuwa Baba yenu vilevile, anayekuwa Mungu wangu na Mungu wenu vilevile.”


Na wakati ule mutafahamu kwamba mimi ni ndani ya Baba yangu, na ninyi ni ndani yangu, na mimi ndani yenu.


Simeoni akamupokea katika mikono, akamushukuru Mungu, akisema:


Mufalme Hezekia na wakubwa wake walipokuja kuangalia mafungu yale, wakamushukuru Yawe na watu wake wa Israeli.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite