Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waefeso 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo. Mimi niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi watu wa Mungu munaokaa Efeso, munaokuwa waaminifu katika kuungana na Yesu Kristo.

Gade chapit la Kopi




Waefeso 1:1
27 Referans Kwoze  

Tunawaandikia ninyi watu wa Mungu munaokaa katika muji Kolosayi, ninyi wandugu munaoungana na Kristo kwa uaminifu. Tunawatakia neema na amani toka kwa Mungu Baba yetu.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo. Mimi ambaye kwa mapenzi ya Mungu, niliitwa kuwa mutume wa Kristo Yesu. Tunawaandikia kanisa la Mungu linalokuwa Korinto na watu wake wote wanaokuwa katika jimbo lote la Akaya.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa wandugu wote wanaokuwa pamoja nami. Ni mimi niliyeitwa kuwa mutume, si kwa kuchaguliwa na watu, wala kwa njia ya mutu, lakini kwa njia ya Yesu Kristo na ya Mungu Baba aliyemufufua. Tunawaandikia ninyi makanisa ya Galatia.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mutumishi wa Kristo Yesu, niliyeitwa na Mungu kuwa mutume na niliyewekwa kwa kazi ya kutangaza Habari Njema yake.


Ninawaandikia ninyi wote wapenzi wa Mungu munaokaa Roma, mulioitwa kuwa watu wake watakatifu. Ninawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.


Tikiko, ndugu yetu mupendwa na mutumishi mwaminifu wa Bwana atawapasha habari zangu zote, kusudi mupate kujua kama mimi ni katika hali gani na namna kazi inavyoendelea.


Ni kwa sababu hii ninawatumia ninyi Timoteo. Yeye ni mwana wangu mupendwa na mwaminifu mbele ya Bwana. Atawakumbusha kanuni ninazofuata katika maisha yangu na Yesu Kristo, nami ninazofundisha fasi zote katika makanisa yote.


Yule anayekuwa mwaminifu katika vitu vichache, yuko mwaminifu vilevile katika vitu vingi. Na yule asiyekuwa mwaminifu katika vitu vichache, hayuko mwaminifu vilevile katika vitu vingi.


Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.


Watapigana vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo pamoja na waaminifu wake aliowaita na kujichagulia atawashinda, kwa sababu yeye ni Bwana wa wabwana na Mufalme wa wafalme.”


Kufuatana na hiyo, Mungu atawabariki wote wanaoamini sawa vile alivyomubariki Abrahamu, mwenye imani.


Basi sasa hakuna azabu kwa wale wanaoungana na Yesu Kristo.


Kisha yeye na watu wa nyumba yake wakabatizwa. Naye akatusihi akisema: “Ikiwa munakubali kweli kwamba ninamwamini Bwana, basi mufike mupange ndani ya nyumba yangu.” Akatulazimisha tuitike.


Ninajua pahali pale unapokaa, ile ndiyo nafasi ya utawala wa Shetani. Wewe unashikamana na jina langu, wala haukuikana imani unayokuwa nayo kwangu, hata wakati Antipa, mushuhuda wangu mwaminifu, alipouawa kati yenu kule kwenye makao ya Shetani.


Lakini juu ya mutumishi wangu Musa, hali ni tofauti kabisa. Yeye ana madaraka ya kuwatunza watu wangu wote.


Tunasumbuka sana tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Wakati tunapotukanwa, tunabariki; wakati tunapoteswa, tunavumilia;


Anania akajibu: “Bwana, nimekwisha kusikia watu wengi wakisema habari za mutu huyo, wakieleza mabaya aliyowatendea watu wako watakatifu wanaokuwa Yerusalema.


Walipofika Efeso, Paulo akawaacha wale wenzake kule. Naye mwenyewe akaingia ndani ya nyumba ya kuabudia na kubishana na Wayuda.


Alipoagana nao, akawaambia: “Kama Mungu akitaka nitarudi huku kwenu tena.” Halafu akaondoka Efeso, akisafiri kwa njia ya chombo.


Kwa maana ninyi wote mumekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani na kuungana na Yesu Kristo.


Kwa hiyo hakuna tena umbalimbali kati ya Wayuda na watu wa mataifa mengine, kati ya watumwa na watu huru, mwanaume na mwanamuke; kwa maana ninyi wote ni mumoja katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.


Kwa sababu hiyo, tangu niliposikia namna munavyomwamini Bwana Yesu na namna munavyowapenda watu wote wa Mungu,


Katika kuungana kwetu na Yesu Kristo, Mungu ametufufua pamoja naye kusudi tutawale pamoja naye mbinguni.


Kwa maana sisi ni viumbe vya Mungu, na kwa kuungana kwetu na Yesu Kristo, alituumba kusudi tuishi maisha ya matendo mema, ambayo Mungu alitutayarishia tangu mbele tupate kuyatenda.


Lakini sasa, katika kuungana kwenu na Yesu Kristo, ninyi muliokuwa mbali, mumekuwa karibu kwa njia ya damu ya Kristo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite