Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 9:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Ndani ya chumba kile kulikuwa chombo cha kufukizia ubani, kilichotengenezwa na zahabu. Na kulikuwa vilevile Sanduku la Agano lililopakaliwa zahabu pande zote. Ndani ya sanduku lile kulikuwa kopo la zahabu lenye mana, na fimbo ya Haruni iliyoota vichipukizi juu yake. Kulikuwa vilevile vibao vya mawe vyenye Maandiko ya Agano la Mungu.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 9:4
26 Referans Kwoze  

Ujitenge na watu hawa, niwaangamize mara moja! Lakini wao wakajitupa uso mpaka chini.


Ndani ya Sanduku la Agano, hamukukuwa kitu kingine isipokuwa tu vile vibao viwili ambavyo Musa aliviweka mule kule Horebu, pahali Yawe alipofanya agano na watu wa Israeli, walipotoka Misri.


Halafu atatwaa chetezo na kutwaa makaa toka kwenye mazabahu mbele ya Yawe na mikono miwili ya ubani uliosagwa vizuri sana na atauleta ndani ya pazia.


Ndani ya hema hilo utaweka lile Sanduku la Agano, kisha weka pazia mbele yake.


Utatundika pazia lile kwenye vifungio, kisha ulete lile Sanduku la Agano mule ndani, nyuma ya pazia lile. Pazia lile litatenga Pahali Patakatifu na Pahali Patakatifu Sana.


Hili lilikuwa onyo kwa Waisraeli kwamba mutu yeyote ambaye si kuhani, maana yake asiyekuwa wa ukoo wa Haruni asiende kwenye mazabahu kwa kumufukizia Yawe ubani. Kama sivyo ataangamizwa kama Kora na wafuasi wake. Haya yote yalitendeka kama vile Yawe alivyomwambia Eleazari kwa njia ya Musa.


Musa alipokuwa anashuka toka kwenye mulima Sinai akiwa na vile vibao viwili vyenye maneno ya agano katika mikono yake, hakujua kwamba uso wake ulikuwa unangaa kwa sababu alikuwa ameongea na Yawe.


Kisha malaika mwingine akakuja kusimama karibu na mazabahu. Alikuwa akishika chetezo cha zahabu. Naye akapewa ubani mwingi kusudi autoe sadaka pamoja na maombi ya watu wote wa Mungu juu ya mazabahu ya zahabu iliyokuwa mbele ya kiti cha kifalme.


Zaidi ya hayo, nimetenga nafasi ya kuweka Sanduku la Agano ambalo ndani yake muko agano Yawe alilofanya na babu zetu, wakati alipowatoa katika inchi ya Misri.”


Hakukukuwa kitu ndani ya Sanduku la Agano lakini vile vibao viwili vya mawe ambavyo Musa aliviweka mule kule Horebu, pahali Yawe alipofanya agano na Waisraeli walipotoka katika inchi ya Misri.


Musa na Haruni wakakwenda, wakasimama mbele ya hema la mukutano,


Sanduku la Agano, miti yake na kiti cha rehema;


Yawe alipomaliza kuongea na Musa juu ya mulima Sinai, akamupatia Musa vile vibao viwili vya mawe ambavyo juu yake Mungu aliziandika zile amri kwa kidole chake mwenyewe.


Kisha Musa akashuka kutoka juu ya mulima akiwa na vile vibao viwili vya agano katika mikono yake, vimeandikwa amri za Mungu pande zote.


Akatengeneza mazabahu ya kufukizia ubani kwa mbao za mujohoro. Mazabahu hiyo ilikuwa ya muraba, sentimetre makumi ine na tano kwa sentimetre makumi ine na tano, na urefu kwenda juu sentimetre makumi tisa. Pembe za mazabahu hiyo zilikuwa kitu kimoja na mazabahu yenyewe.


Nilipopanda juu ya mulima kupokea vibao vya mawe ambavyo kuliandikwa agano ambalo Yawe alifanya nanyi, nilikaa huko siku makumi ine, usiku na muchana; sikukula wala kunywa chochote.


Hakika, nyuma ya siku hizo makumi ine, usiku na muchana, Yawe akanipa vibao hivyo viwili vya mawe ambavyo kuliandikwa agano.


Kisha hekalu la Mungu linalokuwa mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana ndani yake. Halafu kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi, tetemeko la inchi na mvua kubwa ya mawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite