Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 9:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kufuatana na ile, kulikuwa Hema iliyosimikwa. Chumba chake cha kwanza kiliitwa Pahali Patakatifu. Ndani ya chumba kile kulikuwa kinara cha kuwekea taa, meza na mikate iliyotolewa kwa Mungu.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 9:2
21 Referans Kwoze  

Utaingiza meza na kupanga vyombo vyake juu. Utaingiza kile kinara vilevile na kuweka taa zake juu yake.


Ile meza ya mujohoro utaiweka upande wa inje wa pazia lile, na kile kinara cha taa utakiweka upande wa kusini wa hema, kikielekeana na meza. Meza ile itakuwa upande wa kaskazini.


Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, utasimika hema takatifu la mukutano.


Utatundika pazia lile kwenye vifungio, kisha ulete lile Sanduku la Agano mule ndani, nyuma ya pazia lile. Pazia lile litatenga Pahali Patakatifu na Pahali Patakatifu Sana.


Hivi ndivyo utakavyowatendea Haruni na wana wake kufuatana na yote yale niliyokuamuru. Utawatakasa kwa muda wa siku saba,


Haya ndiyo mambo utakayowafanyia Haruni na wana wake kwa kuwatakasa wapate kunitumikia kama vile makuhani. Utatwaa mwana-ngombe dume na kondoo dume wawili wasiokuwa na kilema,


Utatengeneza meza ya mbao za mujohoro yenye urefu wa sentimetre makumi nane na nane, upana sentimetre makumi ine na ine na urefu kwenda juu sentimetre makumi sita na sita.


Meza hiyo utaiweka mbele ya Sanduku la Agano na juu ya meza ile utaweka ile mikate muliyonitolea. Mikate ile itakuwa siku zote mbele yangu.


Utatengeneza kinara cha taa kwa zahabu safi. Tako lake na muti wa kile kinara vitakuwa kitu kimoja, vilevile na vikombe vyake. Mafundo yake na maua yake, vyote vitafuliwa kwa kipande kimoja tu cha zahabu.


Zaidi ya hayo yote, utatengeneza hema takatifu kwa mapazia kumi ya kitani safi iliyosokotwa, na kwa sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu. Mapazia hayo utayapamba kwa makerubi waliochorwa.


Hakuna mutu anayewakisha taa na kuiweka chini ya kitunga, lakini anaiweka juu ya kinara kusudi iwaangazie wote wanaokuwa ndani ya nyumba.


Aliingia ndani ya nyumba ya Mungu na kula mikate mitakatifu iliyotolewa kwa Mungu. Ijapokuwa vile haikuruhusiwa kwake wala kwa watu wake kukula mikate kama ile, isipokuwa makuhani peke yao.


Kuhani Mukubwa wa Wayuda anaingia katika Pahali Patakatifu Sana kila mwaka, akibeba damu ya nyama. Lakini Kristo hakuingia humo kusudi ajitoe mwenyewe sadaka mara nyingi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite