Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 9:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Kwa sababu hii, Kristo ni mupatanishi wa agano jipya. Kwa njia ya kufa kwake aliwakomboa watu toka katika makosa waliyofanya chini ya uongozi wa agano la kwanza, kusudi wale walioalikwa na Mungu wapate kupokea urizi wa milele aliowaahidia.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 9:15
52 Referans Kwoze  

Na wale Mungu aliowachagua tangia zamani, aliwaita vilevile; nao aliowaita, akawahesabia haki, nao aliowahesabia haki, akawatukuzisha vilevile.


Tunajua kwamba katika mambo yote Mungu anatumika kwa kuwajalia wale wanaomupenda, ndio wale walioitwa naye kufuatana na kusudi lake.


Aliingia mara moja tu katika Pahali Patakatifu Sana. Naye hakupeleka mule sadaka ya damu ya mbuzi na ya ngombe, lakini alipeleka damu yake mwenyewe. Na kwa njia ile akatukomboa kwa milele.


Munapaswa kuvumilia, kusudi mutimize mapenzi ya Mungu, na kuweza hivi kupewa kile mulichoahidiwa.


Kwa maana kuna Mungu mumoja tu, na kuna mupatanishi mumoja tu kati ya Mungu na watu, ni yule mutu, Kristo Yesu,


Mumefikia karibu na Yesu anayekuwa mupatanishi wa agano jipya, na kwenye damu yake iliyomwangwa inayosema nasi maneno mema zaidi kuliko damu ya Abeli.


Kwa sababu ya kiapo hiki, Yesu amekuwa kihakikisho kwetu cha agano linalokuwa zuri zaidi.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,


Kwa maana tulipokuwa hatuna uwezo wowote, Kristo alikufa kwa ajili ya waovu kwa wakati uliopangwa.


Hivi vilevile Kristo naye alijitoa kufa mara moja kusudi aondoe zambi za watu wengi. Naye atarudi tena, si kwa ajili ya kuondoa zambi, lakini kwa kuwaokoa wale wanaomungojea.


Wakati Mungu alipomupa Abrahamu ahadi, alifanya vilevile kiapo. Kwa sababu hakuna mutu mwingine mukubwa kuliko yeye kusudi ataje jina lake, akaapa kwa jina lake mwenyewe.


Kwa sababu hiyo, wandugu zangu, ninyi ambao mumeitwa na Mungu na kuwa watu wake kama vile sisi, mufikiri sana juu ya Yesu, anayekuwa mutume na Kuhani Mukubwa wa imani tunayotangaza.


Basi kwa kuwa hao watoto ni wanadamu, wenye mwili na damu, Yesu vilevile alitwaa ile hali ya mwanadamu. Alifanya hivi kusudi kwa njia ya kufa kwake amwangamize Shetani aliyekuwa na uwezo wa kuleta lufu.


Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.


Mungu alipotangaza hilo agano kuwa “jipya”, jambo hilo lilisababisha lile la kwanza kuwa la zamani na lenye kuchakaa. Na kitu chochote kikiwa cha zamani na chenye kuchakaa kinafikia wakati wa kutoweka.


Ilifanyika vile, kusudi kwa neema yake tupate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu na kuupata uzima wa milele tunaotumainia.


Na kwa njia hiyo watapata tumaini la uzima wa milele, ambalo Mungu asiyesema uongo alituahidi mbele ya mwanzo wa nyakati.


Ni kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya watu ambao Mungu alijichagulia kuwa wake, kusudi wao vilevile wapate kuokoka na kupata utukufu wa milele unaopatikana kwa njia ya Kristo Yesu.


Mimi ninawapa uzima wa milele, nao hawatapotea hata milele, wala hakuna mutu anayeweza kuwanyanganya toka katika mukono wangu.


Na kila mutu aliyeacha nyumba yake, kaka, dada, baba, mama, watoto au mashamba kwa ajili yangu, atapokea mara nyingi zaidi na kupewa uzima wa milele.


Na Kristo yeye mwenyewe alituahidi sisi uzima wa milele.


Lakini mukisha kuteswa kwa muda kidogo, Mungu mwenye neema yote aliyewaita kusudi mupate kushiriki naye katika utukufu wake wa milele katika kuungana kwenu na Kristo, yeye mwenyewe atawakamilisha. Atawatia nguvu na kuwasimamisha imara kabisa.


Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.


Watu hawa wote walikufa katika imani pasipo kupokea mambo Mungu aliyoahidi. Lakini waliyaona kwa mbali na kuyafurahia, wakikubali kwamba walikuwa wageni na wasafiri katika dunia.


Mungu amewaalika kuwa vile kwa njia ya Habari Njema tuliyowatangazia, kusudi mupate kushiriki katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.


Kwa maana mushahara wa zambi ni kifo, lakini zawadi Mungu anayotoa ni uzima wa milele kwa kuungana na Yesu Kristo, Bwana wetu.


Katika mambo yenye kuelekea agano la urizi, ni lazima kuhakikisha kwamba yule aliyelifanya amekwisha kufa.


Kwa maana Mungu ndiye aliyetuwezesha kuwa watumishi wa agano jipya, lisilotokana na Sheria iliyoandikwa, lakini na Roho. Sheria iliyoandikwa inaleta kifo lakini Roho analeta uzima.


Ndio sisi tulioitwa naye, si toka kati ya Wayuda tu, lakini toka kati ya watu wa mataifa mengine vilevile.


Basi ikiwa kama tulipokuwa waadui za Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kufa kwa Mwana wake, inaonyesha zaidi sana kwamba tukiwa tumepatanishwa naye, tutaokolewa kwa njia ya uzima wa Kristo.


Lakini Mungu ameonyesha wazi upendo wake kwetu ni wapata gani, kwa maana tulipokuwa tungali wenye zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.


Mutawala mumoja akamwuliza Yesu: “Mwalimu mwema, nifanye nini kusudi nipate uzima wa milele?”


Yesu alipoondoka kwa kuendelea na safari yake, mutu mumoja akamufikia mbio akapiga magoti mbele yake na kumwuliza: “Mwalimu mwema, nifanye nini kusudi nipate kurizi uzima wa milele?”


nilikuwa uchi, mukanipatia nguo; nilikuwa mugonjwa, mukanisaidia; nilikuwa katika kifungo, mulikuja kuniangalia.’


Halafu mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kuume: ‘Mukuje, ninyi muliobarikiwa na Baba yangu; muingie katika Ufalme muliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa dunia.


Kisha majuma hayo makumi saba na mawili, yule aliyepakwa mafuta atauawa na hatabaki na kitu. Muji na Pahali Patakatifu Sana vitaharibishwa na waaskari wa mutawala atakayekuja kushambulia. Mwisho wake utafika kama mafuriko, kukiwa vita na maangamizi kama yalivyopangwa na Mungu.


Yawe anatunza maisha ya watu wakamilifu, na urizi wao utadumu milele.


Kwa njia ya damu ya Kristo, sisi tumekombolewa, maana yake zambi zetu zimesamehewa. Hivi Mungu ameonyesha uwingi wa neema yake


Yeye akawatuma watumishi wake kwa kuwaita watu wale walioalikwa kwa karamu, lakini hawakutaka kufika.


Vilevile kisha kula akatwaa kikombe na kuwapa akisema: “Kikombe hiki ni agano jipya la Mungu, linalohakikishwa kwa njia ya damu yangu.]


“Basi sasa ninawaweka chini ya ulinzi wa Mungu na wa neno lake la neema linaloweza kuwajenga katika imani na kuwapa urizi pamoja na watu wake wote watakatifu.


Lakini ikiwa jambo linaelekea mutu mumoja tu, si lazima kuwa na mupatanishi; na Mungu ni mumoja tu.


Hivi kisha kungojea kwa uvumilivu, Abrahamu akapokea yale Mungu aliyomwahidi.


Muliwahurumia wale waliokuwa katika kifungo, nanyi mulikubali kwa furaha kunyanganywa mali zenu, kwa sababu mulijua kwamba muko na mali inayokuwa bora zaidi na yenye kudumu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite