Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 9:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Hizo ni kanuni za kimutu zinazoelekea vyakula na vinywaji pamoja na desturi mbalimbali za utakaso za kidini. Nazo zinaamuriwa kushikwa mpaka upate kutimia wakati wa kutengeneza vitu vyote upya.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 9:10
32 Referans Kwoze  

Basi, mutu asiwahukumu juu ya chakula au kinywaji, au juu ya kushika sikukuu fulani, ikiwa sikukuu ya Mwandamo wa Mwezi au siku ya Sabato.


Yeye aliondoa Sheria ya Kiyuda pamoja na amri zake na maagizo yake akifanya watu wa jamii hizi mbili kuwa watu wa taifa moja jipya katika kuungana naye na kuleta amani.


Huyu mwingine hakuwekwa kuwa kuhani kwa amri ya kimutu kufuatana na ukoo wake, lakini kufuatana na uwezo wa uzima usiokuwa na mwisho.


Halafu nikamwambia hivi: Ee, Bwana wangu Yawe, sijajichafua hata kidogo kwa kula nyamafu wala nyama aliyeuawa na nyama wa pori, wala sijapata kuonja nyama anayehesabiwa kuwa muchafu tangu ujana wangu.


Kama kati yenu kuna mutu yeyote ambaye ni muchafu kwa sababu ya kutokwa mbegu usiku, huyo atatoka inje ya kambi; hatakaa karibu na kambi.


Ataoga mule katika Pahali Patakatifu na kuvaa nguo zake. Atatoka na kutolea sadaka yake ya kuteketezwa, na sadaka ya kuteketezwa ya watu wa Israeli, kwa kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote.


Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.


Katika agano la kwanza wanasema juu ya kanuni za ibada na juu ya nafasi ya kuabudia iliyojengwa na watu.


wanapokwisha kuonja wema wa Neno la Mungu na nguvu za ulimwengu utakaokuja,


Mungu hakuwapa wamalaika uwezo wa kutawala ulimwengu unaokuja, ndio ule tunaosema juu yake.


Yule mwana-ngombe atakapovunjwa shingo, wazee wote wa muji huo unaokuwa karibu na mutu huyo aliyeuawa, watanawa mikono yao kwa maji juu ya mwana-ngombe


Ataoga mwili wote katika maji, kisha atavaa nguo takatifu. Ataingia pahali pale akiwa amevaa nguo takatifu: koti la kitani na atavaa kapitula ya kitani na akiwa amevaa kanzu ya kitani na kujifunga mukaba wa kitani.


Utamwita Haruni na wana wake wakuje kwenye mulango wa hema la mukutano, kisha uwanawishe.


Musidanganywe na mafundisho mengine ya kigeni ya kila namna. Kwa maana mioyo yetu inapaswa kutiwa nguvu kwa njia ya neema ya Mungu, wala si kwa njia ya kushika kanuni zinazoagizwa juu ya vyakula. Kanuni hizo haziwafalii kitu wale wanaozishika.


Kusudi la mupango ule utakaotimia kwa wakati uliowekwa, ni kukusanya viumbe vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia chini ya utawala wa Kristo.


Lakini sasa munamujua Mungu, au afazali tuseme kwamba sasa munajulikana naye. Basi namna gani mumerudilia tena vitu vinavyotawala dunia, visivyokuwa na uwezo na vikosefu, mukitaka kuwa watumwa tena?


Tena, wanapotoka kwa soko, hawakuli pasipo kuoga kwanza. Na zaidi ya hii wanashika desturi zingine nyingi kama vile namna ya kusafisha vikombe, mitungi na vyungu vilivyotengenezwa na shaba.


mutu huyu, atakuwa muchafu mpaka magaribi na haruhusiwi kula vyakula vitakatifu mpaka pale atakapokuwa ameoga.


Kisha uwapeleke Haruni na wana wake kwenye mulango wa hema la mukutano na kuwanawisha.


basi, asikunywe divai au kileo, asikunywe siki ya divai au ya namna nyingine, asikunywe maji ya zabibu wala kula zabibu zilizoiva au kavu.


Kwa maana wakati ukuhani unapobadilika, Sheria nayo inapaswa kubadilika vilevile.


Lakini nguo ambayo taka limetokea kisha kufuliwa, itafuliwa kwa mara ya pili na hivyo itapata kuwa safi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite