Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 6:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Wakati Mungu alipomupa Abrahamu ahadi, alifanya vilevile kiapo. Kwa sababu hakuna mutu mwingine mukubwa kuliko yeye kusudi ataje jina lake, akaapa kwa jina lake mwenyewe.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 6:13
15 Referans Kwoze  

sawa alivyomwapia babu yetu Abrahamu.


Utatuonyesha uaminifu na wema wako sisi wazao wa Abrahamu na wa Yakobo, kama ulivyowaahidi babu zetu tangu zamani.


Lakini kama hamutatii maneno haya, ninaapa kwa nafsi yangu mwenyewe kwamba nafasi hii itakuwa mabomoko. –Ni ujumbe wa Yawe.


Mimi nimeapa kwa nafsi yangu, ninachosema ni ukweli, neno langu halitarudi nyuma: kila mwanadamu atanipigia magoti, kila mutu atafanya kiapo.


Nitawaangamiza nyama wako wote pembeni ya muto Nili. Maji yake hayatavurugwa tena na mutu wala kwato za nyama kuyachafua tena.


Maana nimeapa kwa nafsi yangu kwamba muji wa Bosira utakuwa kitisho na mushangao, utakuwa uharibifu na kutumiwa kama mufano wa laana; vijiji vyote vitakuwa mabomoko siku zote. –Ni ujumbe wa Yawe.


Uwakumbuke watumishi wako, Abrahamu, Isaka na Israeli, ambao uliwaapia kwa nafsi yako mwenyewe, ukisema: Nitawazidisha wazao wenu kama nyota za mbinguni na inchi yote hii niliyowaahidia nitawapa vizazi vyenu wairizi milele.


Inchi hii yote nimeiweka mbele yenu. Basi, muende kutwaa inchi hiyo ambayo mimi Yawe niliapa kuwapa wazee wenu Abrahamu, Isaka, Yakobo na wazao wao.’ ”


Lakini musikilize neno la Yawe, enyi watu wote wa Yuda munaokaa katika inchi ya Misri. Yawe anasema hivi: Ninaapa kwa jina langu kubwa kwamba hakuna mutu yeyote wa Yuda katika inchi yote ya Misri atakayelitumia jina langu kwa kuapa nalo akisema: Kama vile Bwana wangu Yawe anavyoishi.


Wandugu, nitatumia mufano huu wa kawaida: mutu anapofanya agano kwa njia ya haki, hakuna mutu anayeweza kulivunja au kuongeza neno lingine juu yake.


Lakini, kama zawadi ya Mungu inatokana na Sheria, basi, haiwezi kutokana tena na ahadi. Lakini kwa njia ya ahadi, Mungu ameonyesha wema wake kwa Abrahamu.


Anashika agano alilofanya na Abrahamu, na ahadi aliyomwapia Isaka.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite