Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 4:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Lakini sasa sisi tulioamini, tutaingia kwenye mapumziko ambayo Mungu alitaja aliposema: “Halafu nikaapa kwa kasirani kwamba hawataingia hata kidogo kwenye mapumziko niliyowatayarishia!” Mungu alisema vile ingawa alikuwa amemaliza kazi zake tangu pale alipoumba dunia.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 4:3
15 Referans Kwoze  

Basi, nikaapa kwa kasirani kwamba hawataingia kwenye mapumziko niliyowatayarishia.”


Yeye ndiye aliyechaguliwa na Mungu mbele ya kuumbwa kwa dunia, na alifunuliwa kwa ajili yenu katika nyakati hizi za mwisho.


Ingekuwa hivi, ingemupasa ateswe mara nyingi tangu kuumbwa kwa dunia. Lakini sasa, wakati ukikaribia kwa mwisho, yeye alitokea mara moja tu kusudi awasamehe watu zambi kwa njia ya kujitoa mwenyewe sadaka.


Mbele ya kuumbwa kwa dunia, Mungu alituchagua kuwa watu wake kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watakatifu na pasipo kilema mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,


Mungu akaona kwamba kila kitu alichofanya ni kizuri kabisa. Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya sita.


Basi nikaapa kwa kasirani kwamba hawataingia kwenye mapumziko niliyowatayarishia!”


Ilitokea vile kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii: “Nitasema nao kwa mifano, nitawaambia maneno yaliyofichwa tangu kuumbwa kwa dunia.”


Yeye alikuwa amewaahidia ninyi: Nitawaonyesha ninyi pumziko, nitawapa pumziko enyi muliochoka. Hapa ni pahali pa pumziko. Lakini wao hawakutaka kunisikiliza.


Maana kwa siku sita mimi Yawe niliumba mbingu na inchi, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake, kisha nikapumzika siku ya saba. Kwa hiyo mimi Yawe nilibariki siku ya Sabato, nikaitakasa.


Kwa maana sisi wote tunaishi katika ushirika na Kristo ikiwa tunachunga mpaka mwisho lile tumaini tulilopata kwa mwanzo.


Yawe anasema hivi: Musimame katika masanganjia, muangalie. Muulize juu ya matukio ya zamani. Mutafute pahali panapokuwa njia nzuri muifuate, nanyi mutaweza kupumzika. Lakini wao wakasema: Hatutafuata njia hiyo.


Nitaondoa kati yenu waasi na wale wanaonikosea; nitawaondoa katika inchi walikokaa kama wakimbizi, lakini hawataingia hata kidogo katika inchi ya Waisraeli. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Halafu mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kuume: ‘Mukuje, ninyi muliobarikiwa na Baba yangu; muingie katika Ufalme muliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa dunia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite