Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mujengaji wa nyumba anaheshimiwa zaidi kuliko nyumba yenyewe. Hivi vilevile Yesu anastahili kupewa heshima kubwa zaidi kuliko Musa.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 3:3
11 Referans Kwoze  

Kwa maana sisi tunashirikiana na Mungu katika kazi, na ninyi ni shamba la Mungu. Vilevile ninyi ni majengo ya Mungu.


Lakini mambo tunayoona ndiyo haya: Yesu alifanywa kuwa mwenye cheo chini kidogo ya malaika kusudi kwa neema ya Mungu, Yesu akufe kwa ajili ya watu wote. Na sasa kwa njia ya kile kifo kilichomufikia, amepata utukufu na heshima.


Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana anayesimamia nyumba ya Mungu. Na sisi ndio nyumba ile, kama tukiendelea kuwa na uhodari na kuaminia kupata mambo tunayotumainia.


Yeye ni kichwa cha kanisa linalokuwa mwili wake. Naye ndiye asili ya uzima wa mwili ule. Yeye ndiye mwanzo, muzaliwa wa kwanza, na ndiye aliyefufuka wa kwanza, kusudi akuwe wa kwanza juu ya vyote.


Nami sasa ninakuambia: ewe Petro, wewe ni jiwe, na juu ya jiwe hili, nitajenga musingi wa kanisa langu, na hata uwezo wa lufu hautaweza kulishinda.


Zerubabeli ameuweka musingi wa hekalu naye vilevile atalikamilisha. Hayo yatakapotukia, watu wangu watajua kwamba mimi Yawe wa majeshi ndimi niliyekutuma kwao.


Sheria ile inayoleta kifo imeandikwa neno kwa neno juu ya vibao vya mawe na utukufu wa Mungu ulingaa wakati ule. Uso wa Musa ukangaa vilevile hata Waisraeli hawakuweza kuangalia uso wake ingawa kungaa kule kulikuwa kwa muda tu.


Ni kweli kila nyumba inajengwa na mutu, lakini Mungu ndiye aliyejenga vitu vyote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite