Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 3:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kwa maana sisi wote tunaishi katika ushirika na Kristo ikiwa tunachunga mpaka mwisho lile tumaini tulilopata kwa mwanzo.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 3:14
17 Referans Kwoze  

Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana anayesimamia nyumba ya Mungu. Na sisi ndio nyumba ile, kama tukiendelea kuwa na uhodari na kuaminia kupata mambo tunayotumainia.


Lakini tunatamani sana kwamba kila mumoja kati yenu aendelee kuonyesha bidii ile mpaka mwisho, kusudi mambo yale munayotumainia yapate kutimizwa.


Lakini mufurahi kwa sababu munashiriki katika mateso ya Kristo. Na kwa hiyo mutashangilia kwa furaha wakati atakapoonekana katika utukufu.


Wababa zetu wa kimwili walituadibisha kwa siku chache kufuatana na vile walivyoona kuwa vema. Lakini Mungu anatuadibisha kwa mafaa yetu kusudi tupate kushirikiana naye katika utakatifu wake.


Maana watu wanapokwisha kuangaziwa na ukweli wa Mungu na kuonja zawadi ya mbinguni, na kuishi katika ushirika na Roho Mutakatifu,


Nao mupango ule ni kwamba kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapewa sehemu yao ya urizi kutoka kwa Mungu pamoja na Wayuda. Watu wale ni viungo vya mwili mumoja, nao wanapokea vilevile sehemu ya vitu Mungu alivyoahidi kwa njia ya Yesu Kristo.


Kwa sababu hiyo, wandugu zangu, ninyi ambao mumeitwa na Mungu na kuwa watu wake kama vile sisi, mufikiri sana juu ya Yesu, anayekuwa mutume na Kuhani Mukubwa wa imani tunayotangaza.


Matawi mamoja ya muzeituni uliopandwa yamekatwa, na chipukizi la muzeituni uliojiotesha katika pori umepandikizwa kwenye nafasi yao. Na sasa unafaidia vilevile utomvu unaotoka ndani ya shina la yule muzeituni uliopandwa.


Kwa kuwa mukate ni mumoja, ijapokuwa sisi ni wengi, tuko mwili mumoja, kwa maana sisi wote tunashiriki mukate ule mumoja.


Lile tuliloona na kulisikia, ndilo tunalotangaza kwenu vilevile, kusudi mupate kushirikiana nasi. Na huu ushirika wetu ni ule tunaokuwa nao pamoja na Baba na Mwana wake Yesu Kristo.


Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.


Ninawaonya wazee wa kanisa wanaokuwa kati yenu. Mimi vilevile ni muzee mwenzenu, nami ni mushuhuda wa mateso ya Kristo na zaidi ya hii nitashiriki katika utukufu ule utakaotokea.


Na wale wanaokuwa na wabwana waamini, wasiwakosee heshima kwa sababu wao ni wandugu. Wanapaswa kuwatumikia vizuri zaidi, kwa maana wao ni wandugu waamini na wapendwa, nao wanashiriki faida ya kazi yao. Hayo ndiyo maneno unayopaswa kufundisha na kuhubiri.


Ninafanya hayo yote kwa ajili ya Habari Njema kusudi nipate sehemu ya baraka zake.


‘Hakuna hata mumoja wenu katika kizazi hiki kiovu atakayeingia katika ile inchi nzuri niliyoahidi kuwapa wazee wenu.


Basi ufikiri juu ya wema wa Mungu na ukali wake vilevile. Yeye ni mukali kwa wale walioanguka, lakini yeye ni mwema kwako, ikiwa utaendelea katika wema wake. Kama si vile, wewe vilevile utakatwa.


Kuwa na imani ni kuwa na uhakika juu ya mambo tunayotumainia, ni kusadiki kabisa mambo tusiyoyaona.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite