Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 2:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kwa hiyo ilifaa kwamba Mungu aliyeumba vitu vyote na kuvilinda imara, amufanye Yesu kuwa mukamilifu kwa njia ya mateso, kusudi awalete watoto wengi kuwa washiriki wa utukufu wa Mungu. Kwa maana Yesu ndiye anayewaongoza watu wapate kuokoka.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 2:10
46 Referans Kwoze  

Kwa maana vitu vyote vinatoka kwake, navyo viko kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Atukuzwe hata milele! Amina.


Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


Yesu alitangulia kuingia pahali pale kwa ajili yetu. Amekuwa Kuhani Mukubwa hata milele, kwa mufano wa Melkisedeki.


Mungu alimupa utukufu na kumwikalisha na mamlaka karibu naye na kumuweka kuwa Mutawala na Mwokozi. Na hivi Waisraeli wataweza kugeuka toka zambi zao na Mungu atawasamehe.


akiwaambia: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu kwamba Kristo atateswa na kufufuka kwa siku ya tatu kisha kufa kwake.


Haikumupasa Kristo ateswe kama vile na aingie kwenye nafasi atakapotukuzwa?”


Lakini mukisha kuteswa kwa muda kidogo, Mungu mwenye neema yote aliyewaita kusudi mupate kushiriki naye katika utukufu wake wa milele katika kuungana kwenu na Kristo, yeye mwenyewe atawakamilisha. Atawatia nguvu na kuwasimamisha imara kabisa.


Ingawa hivi, kwa ngambo yetu sisi tuko na Mungu mumoja peke yake tu, ndiye Baba aliyeumba vitu vyote, nasi tunaishi kwa nguvu yake. Vilevile kuko Bwana mumoja tu, ndiye Yesu Kristo. Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, nasi tunaishi kwa nguvu yake.


Sheria ya Musa inawaweka watu wenye uzaifu kuwa Makuhani Wakubwa, lakini kufuatana na kiapo kilichokuja nyuma ya Sheria ile, Mwana anayekuwa mukamilifu kwa milele aliwekwa kuwa Kuhani Mukubwa.


Lakini sasa, kwa njia ya kanisa, watawala na wote wenye uwezo wanaokuwa katika eneo la mbingu wapate kutambua hekima ya Mungu inayokuwa ya namna nyingi.


“Bwana wetu na Mungu wetu, wewe unastahili utukufu, heshima na uwezo, kwa maana wewe ndiwe uliyeumba vitu vyote; vile vimeumbwa na kupata kuwa kutokana na mapenzi yako.”


Ni kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya watu ambao Mungu alijichagulia kuwa wake, kusudi wao vilevile wapate kuokoka na kupata utukufu wa milele unaopatikana kwa njia ya Kristo Yesu.


Kristo ndiye uzima wenu wa kweli, naye atakapoonekana tena, basi ninyi mutaonekana pamoja naye katika utukufu wake.


Kwa maana ninyi wote mumekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani na kuungana na Yesu Kristo.


Sisi wote ambao uso haukufunikwa, tunaonyesha kama kioo utukufu wa Bwana. Kwa hiyo, tunabadilishwa kwa kufanana na Bwana, nasi tunapita toka utukufu mumoja hata utukufu mwingine unaokuwa mukubwa zaidi tena. Kwa maana kazi hii inatimizwa na Bwana ndiye Roho.


Vilevile alitaka kuonyesha uwingi wa utukufu wake kwa wale aliowasikilia huruma; wale ambao alitayarisha tangu zamani kwa kuwatukuzisha.


Halafu mukamwua yule anayekuwa asili ya uzima, lakini Mungu amemufufua. Na sisi ni washuhuda wa jambo hilo.


Yawe ameumba kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya maangamizi.


Kisha mambo haya, nikaangalia nami nikaona mukutano mukubwa sana wa watu wasioweza kuhesabiwa. Kulikuwa watu wa kila taifa, wa kila kabila, wa kila jamaa na wa kila luga. Walikuwa wakisimama mbele ya kiti cha kifalme na mbele ya Mwana-Kondoo, wakivaa kanzu nyeupe na kushika matawi ya muti wa ngazi katika mikono yao.


Ninawaonya wazee wa kanisa wanaokuwa kati yenu. Mimi vilevile ni muzee mwenzenu, nami ni mushuhuda wa mateso ya Kristo na zaidi ya hii nitashiriki katika utukufu ule utakaotokea.


Mungu aliwafunulia wale manabii kwamba ujumbe ule walioutangaza haukuwaelekea wao wenyewe, lakini uliwaelekea ninyi. Na sasa ujumbe ule umetangazwa kwenu na wale waliowahubiri Habari Njema kwa uwezo wa Roho Mutakatifu aliyetumwa toka mbinguni. Hata wamalaika vilevile wanatamani kujua mambo hayo.


Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


Alifanya vile kusudi aonyeshe kwa vizazi vyote vitakavyokuja neema yake kubwa ya ajabu kwa njia ya wema wake katika kuungana kwetu na Yesu Kristo.


Nitakuwa Baba yenu nanyi mutakuwa wana na wabinti wangu. Ni mimi Bwana Mwenye Uwezo ninayesema.”


Mambo haya yote yalifanyika na Mungu, aliyetupatanisha naye kwa njia ya Kristo na kutupatia kazi ya kuongoza watu wengine wapatane naye.


Kwa maana taabu tunayopata ni ndogo na ya muda tu, inatutayarishia utukufu mukubwa sana na wa milele unaokuwa muzuri zaidi kupita mateso haya.


Ninatangaza hekima ya siri ya Mungu, hekima iliyofichwa kwa watu, na iliyopangwa na Mungu mbele ya kuumbwa kwa dunia kwa ajili ya utukufu wetu.


Wakati Yesu alipokwisha kumeza ile divai, akasema: “Yote yametimilika!” Kisha akainamisha kichwa na kukata roho.


Na kufa kwake si kwa ajili ya taifa hili tu, lakini vilevile kwa ajili ya watoto wa Mungu waliosambazwa, kusudi apate kuwaunga katika umoja.)


Yesu akawajibu: “Mwende kumwambia yule mbweha: ‘Leo na kesho nitafukuza pepo na kuponyesha wagonjwa, na kesho kutwa nitamaliza kazi yangu.’


“Sifa kwa Mungu juu mbinguni, na amani katika dunia kwa watu anaowapenda.”


Yule atakayepasua njia atawatangulia, nanyi mutauvunja mulango wa muji na kutoka inje, mutapita na kutoka inje. Mufalme wenu, atawatangulia; Yawe mwenyewe atawatangulia.


Wametafuta wapenzi kati ya watu wa mataifa, lakini mimi nitawakusanya. Na hapo watasikia uzito wa muzigo wa mufalme wa wakubwa.


Mimi nilimufanya kuwa mukubwa na mutawala wa mataifa kusudi yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.


watu niliowaumba kwa ajili yangu mwenyewe, kusudi wazitangaze sifa zangu!


Sizani kama utafanya hivyo, kuwaua watu wa haki pamoja na waovu, kutendea watu wa haki sawa na waovu. Hapana, haiwezekani! Mwamuzi wa dunia yote hataacha kutenda mambo yanayokuwa sawa!”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite