Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 13:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Kwa sababu hii tunaweza kusema kwa uhodari: “Bwana ndiye musaidizi wangu; sitaogopa kitu. Mwanadamu ataweza kunifanya nini?”

Gade chapit la Kopi




Waebrania 13:6
29 Referans Kwoze  

Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


Musaada wetu unatoka kwa Yawe, aliyeumba mbingu na dunia.


Kwa sababu hii, tujongelee kwa uhodari kiti cha kifalme cha Mungu pahali anapowajalia watu neema kusudi apate kutuhurumia na kutujalia neema ya kutusaidia kwa wakati unaofaa.


Ee Mungu Mukubwa, wakati ninapoogopa, mimi ninakutumainia wewe.


Musiwaogope wale wanaoweza kuua tu mwili, lakini wasioweza kuua roho. Lakini zaidi mumwogope Mungu anayeweza kuharibu mwili pamoja na roho katika jehenamu.


Ee Mungu, usikilize maombi yangu; uyategee sikio maneno ya kinywa changu.


Mioyo yetu inamutumainia Yawe. Yeye ni musaidizi wetu na ngao yetu.


Ninakukumbuka ninapokuwa katika kitanda, ninafikiri juu yako usiku kucha,


Yawe asingalinisaidia, ningalikwisha kwenda kwenye inchi ya wafu.


Lakini wanaokutafuta wafurahi na kushangilia. Wanaopenda uwaokoe waseme siku zote: “Yawe ni mukubwa!”


Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Na katika kuungana kwetu na Yesu Kristo na kwa njia ya kumwamini tunapata uhuru wa kufika mbele ya Mungu tukiwa na tumaini kubwa.


Heri yenu ninyi Waisraeli. Nani anayekuwa kama ninyi, watu muliookolewa na Yawe, ambaye ndiye ngao ya musaada wenu, na upanga unaowaletea ushindi! Waadui zenu watakuja wananyenyekea mbele yenu, nanyi mutawakanyaga chini.”


Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu, enyi Waisraeli, musiogope! Nitawasaidia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.


Usinigeuzie mugongo, usinikatae kwa hasira mimi mutumishi wako. Wewe umekuwa siku zote musaada wangu. Usinitupe wala usiniachilie, ee Mungu Mwokozi wangu.


Musiwategemee wakubwa wa dunia; hao ni wanadamu tu, hawawezi kuokoa.


Musa akamalizia kwa kusema: “Ee Israeli, hakuna anayekuwa kama Mungu wako, yeye anayeruka toka mbinguni kuja kukusaidia, anapita juu katika anga katika utukufu wake.


Wa pili aliitwa Eliezeri, kwa vile Musa alisema: “Mungu wa baba yangu ndiye aliyenisaidia nisiuawe na mufalme wa Misri.”


Basi wandugu, tuko na uhodari wa kuingia katika Pahali Patakatifu kwa njia ya damu ya Yesu.


Yonatani akamwambia: “Usiogope, baba yangu Saulo hatakupata. Wewe utakuwa mufalme wa Israeli, mimi nitakuwa wa pili wako. Hata Saulo baba yangu anajua jambo hili.”


Hapo, neno la Yawe lilimufikia Elia kusema hivi:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite