Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 13:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”

Gade chapit la Kopi




Waebrania 13:5
46 Referans Kwoze  

Yawe ndiye anayewaongoza. Yeye atakuwa pamoja nanyi. Yeye hataacha kuwasaidia na hatawatupa. Hivyo, musiogope wala musifazaike.”


Hakuna mutu atakayekushinda siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Musa. Siku zote nitakuwa nawe wala sitakuacha hata kidogo.


Mukuwe imara na hodari, wala musiwaogope au kutishwa nao, maana Yawe, Mungu wenu, ndiye anayekwenda pamoja nanyi. Yeye hataacha kuwasaidia na hatawatupa.”


Kwa heshima ya jina lake kubwa, Yawe hatawatupa watu wake kwa sababu amependa kuwafanya ninyi mukuwe watu wake.


Wamasikini na wakosefu wakitafuta maji lakini hawayapati, wakiwa wamekauka koo kwa kiu, mimi Yawe nitawajibu; mimi Mungu wa Israeli, sitawaacha.


Kisha, mufalme Daudi akamwambia Solomono mwana wake: “Uwe imara na hodari, ufanye kazi hii. Usiogope wala kuwa na wasiwasi. Yawe Mungu ambaye ni Mungu wangu, yuko pamoja nawe. Hatakuachilia lakini atakuwa nawe mpaka itakapomalizika kazi yote ambayo inayohitajika kufanyiwa kwa nyumba ya Yawe.


Nilikuwa kijana na sasa mimi ni muzee; hata kidogo sijaona mutu wa haki ameachwa na Mungu, au watoto wake wakiombaomba chakula.


Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Mimi niko pamoja nawe, nitakulinda popote utakapoenda na kukurudisha katika inchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapotimiza ahadi niliyokupa.”


“Ni kwa sababu hii ninawaambia ninyi: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwa ajili ya chakula au kwa ajili ya kinywaji, wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu kwamba mutavaa nini. Uzima ni wa lazima kuliko vyakula, nao mwili ni wa lazima kuliko nguo.


maana Yawe anapenda haki, wala hawaachi waaminifu wake. Anawalinda hata milele; lakini wazao wa waovu wataangamizwa.


Basi musijisumbue kwa ajili ya kesho, kwa maana kesho itajisumbukia yenyewe. Kila siku ina masumbuko yake inayoitoshelea.


Basi mutupilie mbali mambo yote ya kidunia yanayokuwa ndani yenu: uasherati, uchafu, nia mbaya, tamaa mbaya na tamaa ya mali inayokuwa sawa vile kuabudu sanamu.


Nao waaskari wakamwuliza: “Na sisi, tufanye nini?” Naye akawajibu: “Musifanye ukorofi kwa mutu yeyote wala kumusingizia mutu, lakini mutoshelewe na mishahara yenu.”


Basi, wanakuja kwako makundi kwa makundi na kuikaa mbele yako kama watu wangu, kusudi wasikie unachosema, lakini hawafanyi unachowaambia wafanye. Wanasema kwamba wana upendo, lakini hayo ni kusema tu; wanachotafuta kwa moyo ni faida yao tu.


Uvute moyo wangu kufuata maagizo yako, na si kwa ajili ya kupata faida isiyofaa.


Macho yao yanajaa uzinzi. Wao hawachoki kufanya zambi. Wanavuta watu wasiokamilika. Wanatawaliwa na tamaa za kupata mali. Watu hao wamelaaniwa!


Hapaswi kuwa mulevi wala mupiganaji, lakini akuwe mupole mwenye kupenda amani, wala asikuwe mutu wa kupenda feza.


Mujue waziwazi kwamba mwasherati yeyote na muchafu na mwenye tamaa ya mali (mwenye tamaa ni kama mwenye kuabudu sanamu), hao wote hawatapewa sehemu ya urizi katika Ufalme wa Kristo na Mungu.


Na kwa sababu ya tamaa yao mbaya ya mali, walimu hawa wa uongo watajipatia faida juu yenu kwa njia ya maneno ya uongo. Lakini tangia zamani hukumu yao imekwisha kutangazwa, nao hawatakawia kuangamizwa.


Wote, tangu mudogo mpaka mukubwa kabisa, kila mumoja anatamani kupata faida isiyokuwa ya haki. Tangu manabii mpaka makuhani, kila mumoja wao ni mudanganyifu.


Mwovu anajisifia tamaa zake mbaya, anapata faida kwa njia mbaya, anazarau na kumukataa Yawe.


Musa akakubali kukaa kwa yule mutu. Basi, yule mutu akamupa Musa binti yake anayeitwa Zipora akuwe muke wake.


Kama vile inavyowapasa watu wa Mungu kuishi, tendo lolote la uasherati, la uchafu wala la tamaa ya mali lisisikilike kati yenu.


Lakini niliwaandikia kwamba musishirikiane na mutu anayejiita ndugu mwamini, akiwa mwasherati, mwenye tamaa, mwenye kuabudu sanamu, mutukanaji, mulevi au munyanganyi. Na zaidi ya ile musichangie chakula na mutu wa namna hii.


Na mbegu zilizoanguka katika miiba ni mufano wa wale wanaosikia, lakini masumbuko, utajiri na raha ya dunia vinawasonga hata wanashindwa kutoa matunda yanayokomaa.


uasherati, tamaa mbaya, matendo mabaya, ukorofi, maisha ya ovyo, wivu, matukano, majivuno na upumbafu.


Usitamani nyumba ya mwenzako, wala muke wake, wala mutumwa wake au mujakazi wake, wala ngombe wake, wala punda wake, wala kitu chochote mwenzako anachokuwa nacho.


Ole kwao! Maana wamefuata njia ya Kaina. Kwa ajili ya kupata mali wameanguka katika kosa Balama alilofanya. Wameangamia kwa sababu wameasi kama vile Kora alivyoasi.


wizi, wenye tamaa, walevi, watukanaji, wanyanganyi, watu wale wote hawatapata urizi katika Ufalme wa Mungu.


Wamejaa kila namna ya uovu, ubaya, tamaa na upotovu. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na ukorofi. Wao ni wenye kuchongeana,


Nilipoona vazi moja zuri kutoka Sinari kati ya vitu tulivyonyanganya, vikoroti mia mbili vya feza na furushi ya zahabu yenye uzito wa vikoroti makumi tano vya feza, nikavitamani na kuvitwaa; nikavificha katika udongo ndani ya hema langu; na feza iko chini ya vitu hivyo.”


Yakobo akawaambia: “Unaona kwamba baba yenu hanijali tena kama vile mbele. Lakini Mungu wa baba yangu amekuwa pamoja nami.


Yawe, Mungu wenu, ni Mungu mwenye rehema, hatawaachilia wala kuwaangamiza, wala kusahau agano ambalo alifanya na wazee wenu kwa kiapo.


Wakati mambo haya yatakapokutokea, chochote utakachoweza kufanya ukifanye, maana Mungu yuko pamoja nawe.


Mimi nitakaa kati ya wazao wa Waisraeli, na sitawaacha hata kidogo watu wangu, Waisraeli.”


Yawe, Mungu wetu, akuwe nasi kama alivyokuwa na babu zetu. Tunaomba asituachilie, wala asitutupilie.


Usijichokeshe na kutafuta utajiri; acha kufikiri juu yake.


Nitawaongoza vipofu katika njia wasiyoifahamu, nitawaongoza katika njia ambazo hawazijui. Mbele yao nitaligeuza giza kuwa mwangaza, na pahali penye kuharibika patakuwa laini. Huo ndio mupango wangu wa kufanya, nami nitautimiza.


“Musijiwekee akiba katika dunia hii, pahali nondo na kutu vinapoharibu, nao wizi wanapotoboa nyumba na kuiba.


tunateswa, lakini Mungu hatuachilii; tunatupwa chini, lakini hatuangamizwi.


Labani akamwuliza: “Nikupatie nini?” Yakobo akamujibu: “Hautanipatia kitu chochote. Nitaendelea kuwatunza nyama wako ikiwa utanifanyia jambo hili:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite