Waebrania 13:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Muwakumbuke wale wanaofungwa, mukijisikia sawa vile wenye kufungwa pamoja nao. Vilevile muwakumbuke wale wanaoteswa, mukijisikia sawa vile wenye kuteswa kama wao.
Muliwahurumia wale waliokuwa katika kifungo, nanyi mulikubali kwa furaha kunyanganywa mali zenu, kwa sababu mulijua kwamba muko na mali inayokuwa bora zaidi na yenye kudumu.
Mimi Paulo ninawatumia salamu zangu, nikiziandika kwa mukono wangu mwenyewe. Musisahau kwamba mimi ningali katika kifungo. Ninawatakia neema kutoka kwa Mungu.
Wengine waliuawa kwa kutupiwa mawe, wengine walikatwa vipandevipande kwa misumeno, au kuuawa kwa upanga. Walitangatanga wakivaa ngozi za kondoo au za mbuzi, wakiishi katika umasikini, wakiteswa na kutendewa vibaya.