Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 13:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Musisahau kuwakaribisha wageni, maana kwa kufanya hivi wamoja wamewakaribisha wamalaika pasipo kujua.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 13:2
21 Referans Kwoze  

Kwa maana nilisikia njaa, mukanipa chakula; nilisikia kiu, mukanipa maji; nilikuwa mugeni, mukanikaribisha;


Yawe alimutokea Abrahamu kwenye miti ya mielo ya Mamure. Abrahamu alikuwa anaikaa kwenye mulango wa hema yake wakati wa joto la muchana.


Muwasaidie watu wa Mungu katika mahitaji yao na muwakaribishe wageni.


Mukaribishane ninyi kwa ninyi pasipo kunungunika.


nilikuwa mugeni, nanyi hamukunikaribisha; nilikuwa uchi, nanyi hamukunipatia nguo; nilikuwa mugonjwa na nilikuwa katika kifungo, nanyi hamukukuja kuniangalia.’


Lakini inafaa akuwe mwenye kupenda kukaribisha wageni, mwenye kupenda mema, mukadirifu, mwenye haki, mutakatifu na mutaratibu.


Musafiri hakulala inje ya nyumba yangu; nilimufungulia mulango mupita njia.


Huyo mugeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama vile mwenyeji nawe utamupenda kama vile unavyojipenda mwenyewe, kwa sababu nawe ulikuwa mugeni katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokitendea mumoja wa hawa wandugu zangu wanaohesabiwa kuwa wadogo, mulinitendea mimi.’


Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.


Basi musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja tu, akuwe mukadirifu, mwenye akili, akuwe mwema na mwenye kupenda kukaribisha wageni na mwenye kujua kufundisha.


Gayo, aliyenikaribisha na anayekaribisha kanisa zima kwa kukusanyika kwake, anawasalimia. Erasto, mulinzi wa mali ya muji, pamoja na ndugu yetu Kwarto, wanawasalimia. [


Mafungo ya kweli ni kugawanya chakula chako pamoja na wenye njaa, kuwakaribisha katika nyumba yako wamasikini wasiokuwa na makao, kuwavalisha wasiokuwa na nguo, bila kusahau kuwasaidia wandugu zenu.


Kisha yeye na watu wa nyumba yake wakabatizwa. Naye akatusihi akisema: “Ikiwa munakubali kweli kwamba ninamwamini Bwana, basi mufike mupange ndani ya nyumba yangu.” Akatulazimisha tuitike.


Nilipoona mutu anakufa kwa kukosa nguo, au masikini ambaye hana nguo ya kuvaa,


Siku moja Elisha alikwenda Sunemu, ambako kulikuwa mama mumoja tajiri. Mama yule akamwalika Elisha kwa chakula, na toka siku hiyo ikakuwa kawaida Elisha kula chakula kwake kila mara alipopitia kule.


Wale wamalaika wawili wakafika katika muji wa Sodoma magaribi. Loti alikuwa ameketi kwenye mulango wa muji wa Sodoma. Alipowaona, akasimama kwenda kuwapokea, akainama kwa heshima.


Mupendwa wangu, wewe ni mwaminifu kwa kazi unayofanya kwa ajili ya wandugu, hata kwa wale wanaokuwa wageni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite