Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 13:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Mutii waongozi wenu na kushika maagizo yao. Kwa maana wao wanashugulika kila mara kwa ajili ya roho zenu, na wao wanapaswa kutoa habari ya kazi yao mbele ya Mungu. Kwa kufanya vile mutawaruhusu kufanya kazi yao kwa furaha wala si kwa huzuni, kwa maana haitawafalia kitu kama wakitumika katika huzuni.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 13:17
34 Referans Kwoze  

Wazee wa kanisa wanaoongoza kazi yao vizuri wanastahili kupokea mushahara mara mbili, hasa zaidi wale wanaojitolea kwa kufanya kazi ya kuhubiri na kufundisha.


Muwakumbuke waongozi wenu waliowatangazia neno la Mungu. Muangalie vizuri namna walivyoishi na kufa. Mufuate imani yao.


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.


Na kama musiponisikiliza, moyo wangu utalia machozi kwenye uficho, kwa sababu ya kiburi chenu. Nitalia kwa uchungu na kutoa machozi, maana watu wa Yawe wanapelekwa katika uhamisho.


mukubali kuongozwa na watu kama hawa na wale wote wanaotumika na bidii pamoja nao.


Basi wapendwa wangu, mulionyesha utii wenu siku zote wakati nilipokuwa kwenu, na sasa ingekuwa vema muendelee kufanya vile katika siku hizi ninapokuwa mbali nanyi. Mutumike kwa ajili ya wokovu wenu kwa woga na kutetemeka,


Hivyo Musa akarudi kwa Yawe, akamwambia: Ninasikitika! Watu hawa wametenda zambi kubwa. Wamejifanyia wenyewe miungu ya zahabu.


Basi mumupokee kwa furaha kubwa sana kwa jina la Bwana. Munapaswa kuwapa watu wa namna hii heshima,


Kwa hiyo kila mumoja kati yetu atajitetea mwenyewe kwa Mungu.


Kama mutu hataki kushika maagizo tunayowatolea katika barua hii, mumwangalie vizuri mutu yule, musishirikiane naye, kusudi apate haya.


Muwasalimie waongozi wenu wote na watu wote wa Mungu. Wandugu wa Italia wanawasalimia.


Juu ya kuta zako, ee Yerusalema, nimeweka walinzi, usiku na muchana hawatakaa kimya hata kidogo. Enyi munaomukumbusha Yawe ahadi yake, musikae kimya;


Kwa hiyo wandugu zangu wapendwa, niko na hamu sana ya kuwaona tena. Ninyi ndio munaokuwa furaha yangu na zawadi ya ushindi nitakayopokea. Ninyi wapendwa wangu, ninawaomba musimame imara katika ushirika wenu na Bwana.


Mimi nimewaambia mara nyingi, nami ninawaambia tena kwa machozi: kuna watu wengi wanaoonyesha kwa njia ya mwenendo wao kwamba kufa kwa Kristo juu ya musalaba ni chukizo kwao.


Basi mumutii Mungu. Mupingane na Shetani, naye atawakimbia.


Kila wakati ninapowaombea ninyi, ninaomba kwa furaha,


Halafu bwana wake akamwita na kumwambia: ‘Ni habari gani ile waliyonielezea juu yako? Ninakuomba unifanyie hesabu yote ya mali yangu, kwa sababu hauwezi tena kuwa mulinzi wa mali yangu.’


Sikusikiliza sauti ya walimu wangu, wala kuwategea sikio wale walionifundisha.


Hata hivyo watu walikataa kumusikiliza Samweli, wakasema: “Hapana! Sisi tutakuwa na mufalme juu yetu,


Yule malaika wa Yawe akamwambia: “Rudi kwa bibi mukubwa wako Sarai na umutii.”


mukiwatangazia habari inayoleta uzima. Hivi nitapata sababu ya kujivuna Siku ile ya kurudia kwa Kristo kwa maana itakuwa kitambulisho cha kuhakikisha kwamba bidii yangu na kazi yangu havikupotea bure.


Mukuwe na utii ninyi kwa ninyi kwa kumuheshimu Kristo.


Wewe mwanadamu! Ongea na wanainchi wenzako, uwaambie hivi: Kama nikileta vita katika inchi fulani, na watu wa inchi hiyo wakimuchagua mumoja wao akuwe mulinzi wao,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite