Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 13:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Tena, musisahau kutenda mema na kusaidiana, maana sadaka za namna hii zinamupendeza Mungu.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 13:16
22 Referans Kwoze  

Lakini ninyi, wandugu, musichoke kutenda mema.


Muwasaidie watu wa Mungu katika mahitaji yao na muwakaribishe wageni.


Basi, tunapokuwa bado na wakati, tufanye mema kwa watu wote, na zaidi kwa wandugu zetu katika imani.


Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.


Uwaagize watende mema, wakuwe watajiri katika matendo mazuri, nao wasaidiane kwa moyo safi na kushiriki mali yao na wengine.


Kweli nina vitu vyote vya lazima na zaidi kupita. Sasa kwa kuwa Epafrodito ameniletea zawadi zenu zote, ninatosheka. Zawadi hizi ni kama sadaka ya ubani yenye harufu nzuri, na kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto inayokubaliwa na Mungu na kumupendeza.


Yule aliyekuwa akiiba, asiibe tena, lakini ajikaze kufanya kazi peke yake kwa usawa kusudi apate kuwasaidia wakosefu.


Muangalie vema, hata mumoja wenu asimurudishie mwenzake ubaya kwa ubaya, lakini mutafutiane wema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.


Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.


Yesu aliposikia maneno haya, akamwambia: “Ungali unakosewa na kitu kimoja tu: uuzishe vitu vyote unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudie unifuate!”


Umutumainie Yawe na kutenda mazuri, upate kuishi katika inchi na kuwa salama.


Mupendwa wangu, usifuate mufano mubaya, lakini ufuate mufano muzuri. Mutu anayetenda mema ni mutoto wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hashirikiani na Mungu.


Mwenye kufundishwa Habari Njema anapaswa kushirikiana mapato yake na yule anayemufundisha.


Ninamwomba Mungu kwamba ushirika wa imani yako uzae matunda, na kwa njia hiyo upate kujua mema yote tunayokuwa nayo katika kuungana kwetu na Kristo.


Lakini, mumefanya vizuri kwa kushirikiana pamoja nami katika taabu yangu.


Katika muji wa Yopa kulikuwa mwanafunzi mumoja mwanamuke aliyeitwa Tabita. (Katika kigriki ni “Dorika,” maana yake “Pongo”.) Mwanamuke huyu alikuwa akifanya matendo mengi mema na kuwasaidia wamasikini.


Sadaka ninayokutolea, ee Mungu, ni roho munyenyekevu. Haukatai moyo munyenyekevu na wa kutubu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite