Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 12:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Kwa maana katika vita munayofanya kwa kushinda zambi, hamujapigana bado mpaka kufa.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 12:4
12 Referans Kwoze  

Majaribu yale munayopata, ni yale yanayowapata watu wengine wote. Mungu hatawaachilia kujaribiwa kupita nguvu zenu, kwa maana yeye ni mwaminifu. Jaribu litakapowatokea, atawapatia nguvu ya kulivumilia, hata muweze kulishinda.


Ninajua pahali pale unapokaa, ile ndiyo nafasi ya utawala wa Shetani. Wewe unashikamana na jina langu, wala haukuikana imani unayokuwa nayo kwangu, hata wakati Antipa, mushuhuda wangu mwaminifu, alipouawa kati yenu kule kwenye makao ya Shetani.


Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


Wandugu zetu wamemushinda kwa nguvu ya damu ya Mwana-Kondoo na kwa njia ya ukweli walioshuhudia. Wao walikubali kutoa maisha yao mpaka kufa.


“Halafu watu watawatoa kusudi muteswe na kuuawa, na watu wa mataifa yote watawachukia ninyi kwa ajili yangu.


Muji Babeli umeazibiwa kwa sababu ndani yake kumeonekana damu ya manabii na ya watu wa Mungu pamoja na damu ya watu wote waliouawa katika dunia.


Nikaona kwamba yule mwanamuke amelewa kwa damu ya watu wa Mungu na ya watu waliouawa kwa sababu ya ushuhuda wao kwa ajili ya Yesu. Wakati nilipomwona nikashangaa sana.


Alijinyenyekeza na kutii mpaka kufa, ndiko kufa kwake juu ya musalaba.


Basi tumwendee mbali na kambi, tukikubali kuzarauliwa kama vile yeye alivyozarauliwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite