Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 12:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?

Gade chapit la Kopi




Waebrania 12:25
36 Referans Kwoze  

Kazi wale makuhani wanayofanya ni mufano na kitambulisho kinachoonyesha jinsi mambo kamili yanavyopitika mbinguni. Maneno hayo yanalingana na yale yaliyomutokea Musa. Wakati Musa alipokuwa karibu ya kujenga Hema, Mungu alimwambia: “Ufanye angalisho kusudi upate kutengeneza kila kitu kufuatana na mufano niliokuonyesha kwa mulima.”


Kwa njia ya imani, Noa alionywa na Mungu juu ya mambo yatakayotokea, yale aliyokuwa hajayaona bado. Yeye alimutii Mungu na kujenga chombo kwa kujiokoa yeye mwenyewe pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo yote akahukumu dunia na kupokea haki inayopatikana kwa njia ya imani.


Lakini watu walikataa kunisikiliza, waligeuza mabega na kuziba masikio yao kusudi wasisikie.


Umasikini na mazarau vinamupata yule asiyejali mafundisho, lakini mwenye kusikia maonyo anaheshimiwa.


Lakini mukipotoshwa na kukataa kumusikiliza, mukivutwa kuabudu miungu mingine na kuitumikia,


Yawe akamwambia Musa: Uwaambie Waisraeli: Mumejionea ninyi wenyewe kwamba nimeongea nanyi kutoka mbinguni.


Kisha Yesu akamwambia: “Angalisho, usimwambie mutu neno juu ya hii. Lakini kwenda na kumwonyesha kuhani jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa watu wote kwamba umetakaswa.”


Musikilize mafundisho mupate hekima, wala musiyakatae.


Maana wajinga wanajiua kwa kiburi chao, wapumbafu wanajiangamiza kwa kufanikiwa kwao.


“Nimewaita nanyi mumekataa kusikiliza, nimewanyooshea mukono mukuje nanyi hamukujali,


“Lakini mukiacha kunifuata, na kuasi maongozi yangu na amri nilizowapa, na kwenda kutumikia miungu mingine na kuiabudu,


Lakini watu wote wa Israeli walipoona kwamba mufalme hakuwajali, walimwambia: “Hatuna ushirika wowote na Daudi! Hatuna sehemu yetu kutoka kwa huyo mwana wa Yese. Murudie kwenu, enyi watu wa Israeli! Uitunze nyumba yako mwenyewe, ee Daudi.” Hivyo, watu wa Israeli wakarudi kila mutu kwake.


“Watu wote wa Yawe wanauliza hivi: ‘Ni udanganyifu gani huu mumemufanyia Mungu wa Israeli? Mbona mumemwasi Yawe kwa kujenga mazabahu hii?


Kama ninyi mukikataa kumufuata, yeye atawaachilia tena katika jangwa, nanyi mutasababisha watu hawa wote waangamie.


Mufahamu kwamba mimi Yawe nimewapa siku ya Sabato, ndiyo maana nimewapa chakula cha siku mbili kwa siku ya sita. Basi, kila mutu apumzike ndani ya nyumba yake. Mutu yeyote asitoke katika siku ya saba.”


Watafunga masikio yao wasisikilize mambo ya kweli na kusikiliza hadisi za uongo.


Muangalie vema, hata mumoja wenu asimurudishie mwenzake ubaya kwa ubaya, lakini mutafutiane wema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.


“Huyu Musa ndiye yule Waisraeli waliyemukataa, wakisema: ‘Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi?’ Mungu alimutuma kuwa mukubwa na mukombozi wao, akisaidiwa na yule malaika aliyemutokea katikati ya kichaka kinachowaka moto.


Lakini wakaaji wake wameyaasi maagizo na masharti yangu, wakakuwa wabaya kuliko mataifa na inchi zinazowazunguka. Kweli, wameyakataa maagizo yangu na kuacha kuyafuata masharti yangu.


Wameurudilia uovu wa babu zao ambao walikataa kusikiliza maneno yangu; wanaiabudu miungu mingine na kuitumikia. Watu wa Israeli na watu wa Yuda wamevunja agano nililofanya na babu zao.


Miji yako mitakatifu imekuwa jangwa; Sayuni umekuwa matongo, Yerusalema umekuwa uharibifu.


Wewe uliyasikia na sasa unayaona yote. Kwa nini hauwezi kuyakubali? Tangu sasa nitakujulisha mambo mapya; mambo yaliyofichwa ambayo haukuyajua.


Anayekataa kufundishwa anajizarau mwenyewe, lakini anayekubali maonyo anapata ufahamu.


Tena, ni watu gani waliomukasirikisha Mungu kwa muda wa miaka makumi ine? Si wale wote waliofanya zambi wakaanguka na kufa katika jangwa?


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Lakini akaniambia: “Angalia, usifanye vile! Kwa maana mimi ni mutumishi kama vile wewe, na wandugu zako manabii na watu wanaoshika maneno ya unabii yanayoandikwa katika kitabu hiki. Ni Mungu ndiye unayepaswa kumwabudu!”


Nikaanguka mbele yake kusudi nimwabudu, lakini akaniambia: “Angalia, usifanye vile! Kwa maana mimi ni mutumishi kama vile wewe na wandugu zako wanaoshika ukweli ulioshuhudiwa na Yesu. Ni Mungu ndiye unayepaswa kumwabudu! Maana ukweli ambao Yesu alishuhudia, ndio uwezo unaowaongoza manabii.”


Ninyi mumekwisha kutakaswa kwa njia ya kutii neno la kweli kwa kuwapenda wandugu zenu pasipo unafiki. Basi mupendane kabisa, kwa moyo wenu wote.


Aliwafanya muisikie sauti yake kutoka mbinguni kusudi aweze kuwafundisha; na hapa katika dunia akawafanya muone moto wake mukubwa na kusikia maneno yake kutoka katikati ya moto huo.


Yeyote ambaye hatasikia maneno nabii huyo atakayosema kwa jina langu, mimi mwenyewe nitamwazibu.


Zamani Mungu alisema na babu zetu kwa njia ya manabii, mara nyingi na kwa namna nyingi.


Basi wandugu zangu, muangalie vizuri, kati yenu kusikuwe mutu mumoja mwenye moyo mubaya wa kutokuamini, aliyefikia hata kujitenga mbali na Mungu Mwenye Uzima.


Vilevile juu yake kulisikilika mulio wa baragumu na ngurumo ya sauti. Nao Waisraeli waliposikia sauti ile wakasihi wasiambiwe tena neno,


Nao wakawaendea watu wa makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase kule Gileadi wakawaambia:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite