Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 11:38 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

38 Dunia haikustahili kuwa na watu kama hawa! Walitangatanga katika jangwa na katika milima, wakiishi katika mapango na mashimo ndani ya udongo.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 11:38
16 Referans Kwoze  

na wakati Yezebeli alipowaua manabii wa Yawe, Obadia aliwachukua manabii mia moja, akawaficha makumi tano tano ndani ya pango, akakuwa anawapelekea chakula na maji.


Kule, akafika kwenye pango, akakaa mule. Mara moja Yawe akamutolea ujumbe: “Elia! Unafanya nini hapa?”


Daudi akaondoka kule, akakimbilia kwenye pango karibu na muji wa Adulamu. Kaka zake na wandugu zake wengine waliposikia kwamba alikuwa pale, wote walikwenda kuungana naye.


Mutu wa haki akikufa, hakuna mutu anayejali; mutu mwema akihamishwa toka dunia, hakuna mutu anayefikiri na kusema: Mutu huyo mwema amehamishwa kusudi asipatwe na hasara,


Hauna habari kwamba Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa Yawe, mimi niliwatwaa manabii mia moja nikawaficha makumi tano tano katika pango, nikakuwa ninawapatia chakula na maji?


“Ondoka hapa uelekee upande wa mashariki, ujifiche kwenye kijito cha Keriti kinachokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani.


Wamoja kati ya wanaume kutoka muji wa Zifu wakamwendea Saulo kule Gibea, wakamwambia kwamba Daudi alikuwa anajificha kwenye mulima Hakila, upande wa mashariki wa Yesimoni.


Muchunguze kila upande mujue pahali anapojificha, kisha muniletee habari kamili. Halafu nitakwenda pamoja nanyi na ikiwa angali kule, basi, mimi nitamutafuta kati ya maelfu yote ya watu wa Yuda.”


Saulo alipokuwa angali kule Gibea, Wazifu wakamwendea na kumwambia: “Daudi anajificha katika inchi yetu kwenye makimbilio kule Horeshi, kwenye mulima Hakila, unaokuwa upande wa kusini wa jangwa.


Daudi alijua kwamba Saulo alitaka kuyaangamiza maisha yake. Daudi akabaki katika mbuga za Zifu, kule Horeshi.


Wamidiani waliwagandamiza sana Waisraeli, mpaka wakajichimbia mashimo na mapango kwenye milima kuwa makimbilio yao.


Kisima ambamo Isimaeli alitupa maiti za wale watu aliowaua ni kile kikubwa ambacho mufalme Asa alikuwa amekichimba kwa kujikinga na Basha, mufalme wa Waisraeli. Isimaeli mwana wa Netania alikijaza kisima hicho maiti za wale watu aliowaua.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite