Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 11:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 walizimisha moto mukali, waliponyoka kuuawa kwa upanga. Walikuwa wazaifu, lakini wakapata nguvu; walikuwa shujaa katika vita na kushinda majeshi ya kigeni.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 11:34
36 Referans Kwoze  

Basi, akawashambulia vikali na kuwaua wengi. Kisha akaenda kuishi katika pango la Etamu lililokuwa chini ya jiwe.


Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.


wewe unayewapa wafalme ushindi, unayemwokoa mutumishi wako Daudi!


Halafu akatuma mujumbe kwenda kumuleta Elisha. Wakati uleule, Elisha alikuwa ndani ya nyumba pamoja na wazee waliomutembelea. Mbele ya kufika kwa mujumbe wa mufalme, Elisha akawaambia wazee: “Yule mwuaji amemutuma mutu kuja kunikata kichwa! Atakapofika hapa, mufunge mulango, wala musimuruhusu aingie. Vilevile bwana wake anamufuata nyuma.”


Elia akakimbilia katika muji wa Beri-Seba katika jimbo la Yuda, kule alikomwacha mutumishi wake,


Wandugu wapendwa, musishangae kwa kuona mateso makubwa ya kuwajaribu munayopata. Musiyahesabu kuwa kitu kigeni kwenu.


Lakini Yeremia alikuwa akilindwa na Ahikamu mwana wa Safamu kusudi asitiwe katika mikono ya watu na kuuawa.


Umewaacha watu watukanyage; tumepitia katika moto na katika maji. Lakini sasa umetuleta kwenye usalama.


Macho yangu yamechoka kwa huzuni; yamefifia kwa kutaabishwa na waadui.


Nyuma ya Yobu kuwaombea warafiki zake, Yawe akamurudishia Yobu hali yake ya kwanza. Akamupa mara mbili ya yote aliyokuwa nayo pale mbele.


Atakuepusha toka kifo wakati wa njaa, toka mapigo ya upanga wakati wa vita.


Daudi alikimbia kutoka Nayoti katika Rama, akaenda mpaka kwa Yonatani, akamwambia: “Nimefanya nini? Kosa langu ni gani? Nimemutendea baba yako zambi gani hata anajaribu kuyaangamiza maisha yangu?”


Wa pili aliitwa Eliezeri, kwa vile Musa alisema: “Mungu wa baba yangu ndiye aliyenisaidia nisiuawe na mufalme wa Misri.”


Basi, alimutupia Daudi mukuki mara mbili maana alifikiri: “Nitamubanisha Daudi kwenye ukuta.” Lakini Daudi aliepa mara zote mbili.


Saulo alijaribu kumuchoma Daudi kwa mukuki ule. Lakini Daudi aliepa mukuki wa Saulo na mukuki ukapiga ukuta. Daudi akakimbia na kutoroka.


Mufalme Ahabu alimwelezea muke wake Yezebeli mambo yote Elia aliyofanya na jinsi alivyowaua manabii wa Bali kwa upanga.


Siku moja, wanafunzi wa manabii walimulalamikia Elisha wakisema: “Pahali hapa tunapokaa ni padogo sana kwetu!


Tumeponyoka kama ndege katika mutego; mutego umefyatuka, nasi tukaponyoka.


Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite