Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 11:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Watu hawa wote walikufa katika imani pasipo kupokea mambo Mungu aliyoahidi. Lakini waliyaona kwa mbali na kuyafurahia, wakikubali kwamba walikuwa wageni na wasafiri katika dunia.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 11:13
36 Referans Kwoze  

Kwa njia ya imani, Musa alitoka katika inchi ya Misri bila kuogopa kasirani ya mufalme. Na kama vile mutu mwenye kumwona Mungu asiyeonekana, yeye hakurudi nyuma.


Unapomwazibu mutu zambi zake kwa kumwadibisha, unaharibu kama nondo kile anachokipenda. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


“Mimi ninaishi kama mugeni kati yenu. Munipatie sehemu ya udongo ya kaburi, kusudi nipate kumuzika marehemu muke wangu.”


Baba yenu Abrahamu alishangilia akitumainia kuona siku ya kuja kwangu; na wakati alipoiona, alifurahi.”


Watu hawa wote walishuhudiwa vizuri na Mungu kwamba wamemupendeza kwa njia ya imani yao. Lakini hawakupokea mambo yale Mungu aliyowaahidia,


Basi sasa, ninyi watu wa mataifa mengine si wageni tena wala wapangaji. Lakini sasa mumekuwa wanainchi pamoja na watu wa Mungu na tena mumekuwa watu wa jamaa la Mungu.


Kwa maana tumeokolewa, lakini ni kwa tumaini. Mutu akiona kitu anachokitumainia, hilo si tumaini tena, kwa maana nani anayeweza kuendelea kutumainia kitu anachokiona?


Wapendwa wangu, ninawasihi ninyi, kama vile wageni na wasafiri hapa katika dunia, muepuke tamaa za mwili zinazopigana na roho.


Na ikiwa katika maombi yenu munamwita “Baba” yule anayehukumu kila mutu pasipo upendeleo kufuatana na matendo yake, basi muishi katika heshima mbele yake kwa muda unaowabakilia kwa kuishi hapa katika dunia.


Alifanya vile kwa sababu alijua hakika kwamba yule aliyetoa ahadi ile yuko na uwezo wa kuitimiza.


Ninajua wazi Mukombozi wangu anaishi. Kwa mwisho yeye atasimama hapahapa katika dunia.


“Ee Yawe, ninangojea uniokoe!


Yakobo akamujibu: “Umri niliojaliwa kama musafiri ni miaka mia moja na makumi tatu. Miaka hiyo imekuwa michache na iliyojaa mateso, tena haijafikia hesabu ya miaka wazee wangu waliyoishi kama wasafiri.”


Kisha kuishi maisha marefu na ya fanaka, akakufa na kukutana na wazee wake.


Kwa njia hii tutatambua kwamba sisi ni watu wa ukweli, na mioyo yetu itatulia mbele ya Mungu.


Kweli ninawaambia: manabii wengi na wenye haki wengi walitamani kuona mambo munayoona, lakini hawakuyaona, na kusikia maneno munayosikia, lakini hawakuyasikia.


Yakobo alipomaliza kuwaagiza wana wake, akarudisha miguu yake juu ya kitanda, akakufa na kukutana na wazee wake.


Mimi ni mugeni tu hapa katika dunia; usinifiche amri zako.


Ninamwona atakayekuja, ninamwona, lakini hayuko karibu. Nyota itatokea kwa wazao wa Yakobo, atatokea mufalme kati ya Waisraeli. Kwa fimbo yake atapiga viongozi wa Wamoabu, atawaangamiza wazao wote wa Seti.


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


Isaya alisema maneno haya kwa sababu aliona kwa mbali utukufu wa Yesu, naye alisema habari zake.


Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”


Hayo ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hayo ndiyo maneno baba yao aliyowaambia alipowabariki, kila mumoja wao kama alivyostahili.


Kisha Israeli akamwambia Yosefu: “Kama vile unavyoona, mimi niko karibu kufa. Hata hivyo, Mungu atakuwa pamoja nanyi, na kuwarudisha katika inchi ya babu zenu.


Zipora akamuzalia mutoto mwanaume. Musa akasema: “Nimekimbilia katika inchi ya kigeni”, kwa hiyo akamupa yule mutoto jina Gersomi.


Musiuzishe mashamba kabisa, maana hiyo ni mali yangu na ninyi ni wageni na wasafiri katika inchi yangu.


Maana sisi hatuangalii vitu vile vinavyoonekana, lakini vitu visivyoonekana. Kwa sababu vile vinavyoonekana vinadumu muda kidogo tu, lakini vile visivyoonekana, vinadumu milele.


Basi tuna uhodari siku zote. Tunajua kwamba wakati tunapoishi katika mwili huu, tunaishi mbali na makao ya Bwana.


Maana watu wanaosema maneno kama haya wanaonyesha wazi kwamba wanatafuta inchi yao wenyewe.


Kwa njia ya imani, Abrahamu alimutoa Isaka kama vile sadaka wakati Mungu alipopima imani yake. Abrahamu alikubali kumutoa mwana wake wa pekee, ingawa ni yeye ndiye aliyekuwa amepewa ahadi na Mungu.


Barua hii inatoka kwangu mimi Petro, mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi muliochaguliwa na Mungu na ambao mulisambazwa, na munaoishi kama wakimbizi kule Ponto, Galatia, Kapadokia, Azia na Bitinia.


Abrahamu alikaa katika inchi ya Wafilistini muda murefu.


Lakini Hobabu akajibu: Mimi sitakwenda nanyi; lakini nitarudi katika inchi yangu na kwa wandugu zangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite