Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 10:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 kwa sababu damu ya ngombe na ya mbuzi haiwezi kuondoa zambi.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 10:4
19 Referans Kwoze  

Kila kuhani anasimama mbele ya Mungu kila siku kwa kufanya ibada na kutoa sadaka za namna moja mara nyingi zisizoweza hata kidogo kuondoa zambi.


Ninyi munajua kwamba Yesu Kristo alikuja kusudi aondoe zambi, na hakuna zambi ndani yake.


Na hili ndilo agano nitakalofanya nao, wakati nitakapowasamehe zambi zao.”


Kwanza Kristo alisema: “Haukutaka wala haukupendezwa na sadaka na matoleo, wala sadaka za kuteketezwa kwa moto wala sadaka za kusamehewa zambi.” (Alisema vile ingawa sadaka hizo zote zilitolewa kufuatana na maagizo ya Sheria.)


Huo ni mufano wa wakati wa sasa unaoonyesha kwamba matoleo na sadaka zinazotolewa kwa Mungu haziwezi kumufanya yule anayeabudu kuwa na moyo mukamilifu.


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Na mutu anapaswa kumupenda Mungu kwa moyo wake wote, kwa akili yake yote na kwa nguvu yake yote, naye anapaswa kumupenda mwenzake kama vile anavyojipenda mwenyewe. Mambo hayo ni bora zaidi kuliko kumutolea Mungu nyama za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine zote.”


Maana kitu ninachotaka kwenu ni wema na si sadaka, kumujua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto.


Uniokoe kutoka kosa la kumwanga damu, ee Mungu, Mungu mwokozi wangu, nami nitaimba kwa sauti kwamba umeniokoa.


Enyi Waisraeli, mumurudilie Yawe, Mungu wenu. Mumejikwaa kwa sababu ya uovu wenu.


Kwa nini kuniletea ubani kutoka Seba, na udi wa harufu nzuri kutoka inchi ya mbali? Sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto hazikubaliki, wala sadaka zenu zingine hazinipendezi.


Lakini watu hawa wanafanya wanavyotaka: wananitolea sadaka ya ngombe na tena wanaua watu kwa kutambikia. Wananitolea sadaka ya mwana-kondoo na vilevile wanaua imbwa. Wananitolea sadaka ya unga na vilevile wanatolea damu ya nguruwe. Wanachoma ubani mbele yangu na kwenda kuabudu miungu ya uongo. Hao wamechagua kufuata njia zao wenyewe.


Sheria ya Kiyuda ni mufano wa mema yatakayotokea, lakini si kitambulisho kinachoonyesha mambo yale kamili. Kwa sababu hii Sheria haiwezi hata mara moja, kwa njia ya sadaka zinazotolewa mara nyingi kila mwaka, kuwafanya wakamilifu wale wanaomwendea Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite