Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 10:38 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

38 Mwenye haki mbele yangu ataishi kwa njia ya imani. Lakini kama akirudi nyuma, sitapendezwa naye.”

Gade chapit la Kopi




Waebrania 10:38
24 Referans Kwoze  

Na zaidi ya hii ni wazi kwamba hakuna mutu anayehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya Sheria. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mwenye haki ataishi kwa njia ya imani.”


Kwa maana Habari Njema inaonyesha namna Mungu anavyowahesabia watu haki mbele yake. Jambo hilo haliwezekani isipokuwa kwa njia ya kuamini tu. Ni sawa vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu yanayosema: “Mwenye haki ataishi kwa njia ya imani.”


Andika: Uwaangalie wenye kiburi, hao wataangamia; lakini wenye haki wataishi kwa kumwamini Mungu.


Utuonyeshe wema wako, ee Yawe, utujalie wokovu wako.


Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


lakini anapendezwa na watu wanaomuheshimu, ndio wanaotegemea wema wake.


Lakini halizami ndani yao kama mizizi. Wanalishika kwa muda mufupi tu. Wakati taabu na mateso vinapowafikia kwa ajili ya Neno la Mungu, mara moja, wanaanguka.


“Muangalie, mutumishi wangu niliyejichagulia, anayekuwa mupendwa wangu, ninayependezwa naye. Nitamujaza Roho wangu, naye atatangaza haki yangu kwa mataifa.


Tena, kama mutu wa haki akigeuka katika haki yake na kutenda uovu, nami nikimwekea kikwazo, mutu huyo atakufa. Kwa vile haukumwonya, atakufa kwa sababu ya zambi yake, nayo matendo yake ya haki hayatakumbukwa. Lakini wewe utabeba lazima ya damu yake.


Ndio wale waliomwua Bwana Yesu na manabii, wakatutesa sisi vilevile. Wao hawamupendezi Mungu, nao ni waadui za watu wote!


Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.


Nitawaangamiza wote walioniacha mimi Yawe, wote walioacha kunitafuta na kuniuliza shauri.


Lakini, mutu wa haki akiacha haki yake na kutenda uovu na kufanya machukizo yaleyale mutu mwovu anayofanya, basi, huyo ataishi? Hapana! Matendo yake yote mema aliyotenda hayatakumbukwa tena; atakufa kwa sababu ya uasi na zambi aliyotenda.


Maana Yawe anapendezwa na watu wake; yeye anawaheshimisha wanyenyekevu kwa kuwapa ushindi.


Ee Yawe, kwa mapambazuko unasikia sauti yangu, asubui ninakutolea sadaka yangu, kisha ninangojea unijibu.


Watu hawa wametoka kati yetu, lakini hawakukuwa wa kundi letu, na kwa sababu hii wametuacha. Kama wangekuwa wa kundi letu, wangekaa pamoja nasi. Lakini wametuacha kusudi ionekane wazi ya kama hawakukuwa wa kundi letu.


Mimi ninamwahidi mutu wa haki kwamba ataishi; lakini yeye akiamini kwamba haki yake inatosha, akianza kutenda uovu, matendo yake yote mema ya zamani hayatakumbukwa; atakufa kwa uovu wake.


Lakini sisi si watu wenye kurudi nyuma na kupotea, lakini sisi ni watu wenye imani na wenye kuokoka.


Mumewahukumu na kuwaua wenye haki, nao hawakupingana nanyi.


Maana nimefuata njia za Yawe, wala sikujitenga na Mungu wangu kwa ajili ya uovu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite