Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 10:33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

33 Kwa ngambo moja mulitukanwa na kuteswa waziwazi mbele ya watu. Na kwa ngambo ingine mulishirikiana na wale waliotendewa vibaya.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 10:33
19 Referans Kwoze  

Kwa maana inaonekana kuwa Mungu ametufanya sisi mitume kuwa watu wenye hali ya chini kabisa. Tunahesabiwa kama watu wanaohukumiwa kufa mbele ya watu. Tumewekwa kama kitu cha kushangaza, kinachoangaliwa na dunia nzima, nao wamalaika na watu vilevile.


Lakini, mumefanya vizuri kwa kushirikiana pamoja nami katika taabu yangu.


Ni haki kwangu kuwa na mafikiri haya kwa ajili yenu ninyi wote, kwa sababu ninawakumbuka kila mara. Kwa maana mumeshiriki pamoja nami katika neema ile Mungu aliyonipatia, ingawa sasa niko katika kifungo hata na wakati nilipokuwa huru kutetea na kuimarisha Habari Njema.


Wengine walichekelewa na kupigwa fimbo, na wengine walifungwa minyororo na kutupwa katika kifungo.


Wandugu, mambo yale yale yaliyotokea makanisa ya Mungu ya Yudea yanayoungana na Yesu Kristo, ndiyo yaliyowatokea ninyi vilevile. Kwa maana ninyi muliteswa na wanainchi wenzenu kama vile wao walivyoteswa na wanainchi wenzao Wayuda.


Munisikilize, enyi munaojua mambo ya haki, ambao sheria zangu ziko ndani ya mioyo yenu. Musiogope mazarau ya watu, wala kufazaishwa na masimango yao.


Ee Mungu, simama sasa ujitetee! Ukumbuke mazarau ya kila siku ya wasiokujua.


Basi tumwendee mbali na kambi, tukikubali kuzarauliwa kama vile yeye alivyozarauliwa.


Aliona kwamba kupatishwa haya kwa ajili ya Kristo kuna faida kubwa zaidi kuliko kupata utajiri wote wa inchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia kupokea zawadi yake.


Basi, usisikie haya ya kutoa ushuhuda kwa ajili ya Bwana wetu, wala usisikie haya kwa sababu yangu mimi ninayekuwa katika kifungo kwa ajili yake. Lakini ushiriki nami katika mateso kwa ajili ya Habari Njema, kufuatana na uwezo unaopewa na Mungu.


Kwa sababu hii ninafurahia uzaifu, matusi, ukosefu, taabu na mateso kwa ajili ya Kristo. Kwa maana wakati ninapokuwa muzaifu, basi ndio wakati ule ninapokuwa na nguvu.


Sasa sikiliza kwa uangalifu, ewe Yoshua, Kuhani Mukubwa; musikilize vilevile enyi makuhani wenzake munaokuwa pamoja naye, ninyi munaokuwa kitambulisho cha wakati muzuri unaokuja: Nitamuleta mutumishi wangu anayeitwa Tawi.


Nitakutupia uchafu, na kukuzaraulisha, na kukufanya kuwa mushangao kwa watu.


Ee Bwana, ukumbuke matusi ya mutumishi wako, jinsi ninavyovumilia mazarau ya mataifa.


Ee Bwana, uwalipize mataifa jirani mara saba kwa ajili ya matusi waliyokutukana.


Kwa wengi nimekuwa mushangao, lakini wewe ni kimbilio langu lenye nguvu.


Nimekuwa mugeni kwa wandugu zangu, kaka na dada zangu hawanitambui.


Kwa maana katika vita munayofanya kwa kushinda zambi, hamujapigana bado mpaka kufa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite