Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 10:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Mutu yeyote aliyevunja Sheria ya Musa, aliuawa bila huruma kisha ushuhuda wa watu wawili au watatu.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 10:28
17 Referans Kwoze  

Ujumbe wa Sheria uliotangazwa na malaika ulitimizwa, na hata kila mutu aliyekosa kuufuata na kuasi aliazibiwa sawa inavyostahili.


“Ushuhuda wa mutu mumoja hautoshi kwa kuhukumu mutu juu ya kosa lolote au uovu juu ya kosa lolote alilofanya. Ni ushuhuda wa watu wawili au watatu tu ndio utakaohakishwa.


Hii ni safari yangu ya tatu ninayotayarisha kuja kwenu. Kama Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Kila neno linapaswa kuhakikishwa kwa ushuhuda wa watu wawili au watatu.”


Na imeandikwa hata katika Sheria yenu kama ushuhuda wa watu wawili ni wa kweli.


Lakini kama akikataa kukusikia, utwae mutu mumoja au wawili na kumwendea pamoja nao, kusudi kila neno lihakikishwe kwa ushuhuda wa watu wawili au watatu, sawa vile Maandiko Matakatifu yanavyosema.


Basi, Daudi akamwambia Natani: “Nimetenda zambi mbele ya Yawe.” Natani akamwambia: “Yawe amekusamehe zambi yako, nawe hautakufa.


Musimwonee huruma, lakini mutakomesha uovu wa mauaji ya mutu asiyekuwa na kosa katika Israeli, kusudi mupate kuishi kwa amani.


Basi, watu wakamutoa inje ya kambi, wakamupiga mawe mpaka akakufa, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


Kwa maana anamwambia Musa: “Nitamuhurumia yule ninayependa kumuhurumia; nitamurehemu yule ninayependa kumurehemu.”


Nitawagonganisha wao kwa wao hata baba na watoto. –Ni ujumbe wa Yawe.– Sitawahurumia, sitawaachilia wala sitawarehemu, mpaka nitakapowaangamiza.


Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.


Kwa nini basi, umezarau neno langu mimi Yawe na kufanya uovu huu mbele yangu? Umemwua Uria wa Hiti kwa upanga, ukamukamata muke wake kuwa muke wako. Umewatumia Waamoni kwa kumwua Uria katika vita!


Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite