Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waebrania 10:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.

Gade chapit la Kopi




Waebrania 10:22
66 Referans Kwoze  

Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mutakuwa safi. Nitawatakasa toka uchafu wenu wote na toka uchafu wa sanamu za miungu yenu yote.


Yesu akajibu: “Kweli, kweli ninakuambia: mutu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu.


Maji haya ni mufano wa ubatizo unaowaokoa ninyi sasa. Ubatizo ule si kwa ajili ya kusafisha uchafu wa mwili lakini ni njia ya kufanya mapatano na Mungu katika zamiri safi. Nao unawaokoa ninyi kwa njia ya ufufuko wa Yesu Kristo,


Alifanya hivi kusudi atakase kanisa kwa ajili ya Mungu, akilisafisha kwa maji na kwa neno.


Na wamoja kati yenu walikuwa kama wao. Lakini mumesafishwa toka zambi, mumetakaswa na kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu.


kwa maana Sheria ya Musa haikuleta ukamilifu. Lakini sasa kumeletwa tumaini nzuri zaidi, na kwa njia ya tumaini hili tunaweza kumukaribia Mungu.


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


Kwa sababu hii, tujongelee kwa uhodari kiti cha kifalme cha Mungu pahali anapowajalia watu neema kusudi apate kutuhurumia na kutujalia neema ya kutusaidia kwa wakati unaofaa.


Mumefikia karibu na Yesu anayekuwa mupatanishi wa agano jipya, na kwenye damu yake iliyomwangwa inayosema nasi maneno mema zaidi kuliko damu ya Abeli.


alituokoa sisi. Hakufanya vile kwa sababu ya matendo yetu ya haki, lakini alituokoa kwa sababu ya huruma yake kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetuwezesha kuzaliwa mara ya pili na kuwa na maisha mapya kwa kutusafisha kwa maji.


Lakini, kwangu ni vizuri kuwa karibu na Mungu. Wewe Bwana wangu Yawe ndiwe usalama wangu. Nitatangaza mambo yote uliyotenda!


Mungu Baba aliwachagua ninyi tangu mbele kufuatana na mupango wake na kufanywa watakatifu na Roho, mupate kumutii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Ninawatakia neema na amani kwa uwingi.


Na katika kuungana kwetu na Yesu Kristo na kwa njia ya kumwamini tunapata uhuru wa kufika mbele ya Mungu tukiwa na tumaini kubwa.


Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia. Musafishe mikono yenu, ninyi wenye zambi! Mutakase mioyo yenu, ninyi wenye nia mbili!


Kwa maana, kwanza Musa aliwatangazia watu wote amri zote za Sheria. Kisha akatwaa damu ya ngombe pamoja na maji, naye akavinyunyiza juu ya kitabu cha Sheria na juu ya watu wote akitumia manyoya mekundu na vitawi vya muti wa hisopo.


Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu.


Kisha nikatwaa maji, nikakukogesha kwa kusafisha damu uliyokuwa nayo, nikakupakaa mafuta.


Nitawapa moyo wa kujua kwamba mimi ndimi Yawe. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; maana watanirudilia kwa moyo wao wote.


Halafu Musa akawaleta Haruni na wana wake na kuwanawisha.


Lakini inafaa aombe kwa imani pasipo kuwa na mashaka. Kwa maana mutu anayekuwa na mashaka anafanana na zoruba katika bahari inayosukumwa na upepo na kutupa maji huku na huko.


Mwana wangu, unisikilize kwa uangalifu, ufuate mwenendo wa maisha yangu.


Nitakusifu kwa moyo wenye kunyooka, nikijifunza maamuzi yako ya haki.


Unijaze furaha na shangwe, unifurahishe tena, mimi ambaye uliniponda.


Hivi ndivyo utakavyowatakasa: uwanyunyizie maji ya utakaso kisha uwaambie wajinyoe mwili muzima, wafue nguo zao na kujitakasa.


Kisha, atamunyunyizia yule mwenye kutakaswa ile damu mara saba, halafu atamutangaza mutu huyo kuwa safi. Atamwacha yule ndege muzima aende zake katika pori inje ya muji.


Kwa njia ya imani, alianzisha sikukuu ya Pasaka, na kuamuru damu inyunyizwe, kusudi malaika mwangamizaji asiwaue wazaliwa wa kwanza wanaume wa Waisraeli.


Basi wandugu, tuko na uhodari wa kuingia katika Pahali Patakatifu kwa njia ya damu ya Yesu.


Siku hiyo, kutatokea chemichemi ya kutakasa zambi na uchafu wa wazao wa Daudi na wakaaji wote wa Yerusalema.


Bwana anasema: Watu hawa wanakuja kuniabudu kwa maneno tu, lakini mioyo yao iko mbali nami. Wananiheshimu kulingana na desturi ya watu tu, jambo walilojifunza wao wenyewe.


“Nawe Solomono mwana wangu, umujue Mungu wa baba yako, na umutumikie kwa moyo wako wote na kwa nia nzuri; yeye Yawe anachunguza mioyo na anafahamu mipango na mafikiri ya mwanadamu. Ukimutafuta yeye, utamwona; lakini ukimwacha, atakutupilia mbali milele.


Kisha uwapeleke Haruni na wana wake kwenye mulango wa hema la mukutano na kuwanawisha.


Hizo ni kanuni za kimutu zinazoelekea vyakula na vinywaji pamoja na desturi mbalimbali za utakaso za kidini. Nazo zinaamuriwa kushikwa mpaka upate kutimia wakati wa kutengeneza vitu vyote upya.


Wanadanganywa na watu wenye uongo na wanafiki wenye zamiri iliyokufa, iliyoharibika kabisa kama vile imeteketezwa kwa moto.


Mwongozi wao atakuwa mumoja wao, mutawala wao atatokea katikati yao. Nitamuruhusu kuwa karibu nami; maana, ni nani anayeweza kusubutu kuhatarisha uzima wake kwa kunikaribia? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Pamoja na hayo yote, Yuda, dada mudanganyifu wa Israeli hakunirudilia kwa moyo wote, lakini kwa unafiki tu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini sasa ameyashangaza mataifa mengi. Wafalme watapumbazika kwa sababu yake, maana wataona mambo ambayo hawajapata kuambiwa, na kufahamu mambo ambayo hawajapata kusikia.


Ninakulilia kwa moyo wangu wote; unijibu, ee Yawe, nifuate masharti yako.


na kutoka kwa Yesu Kristo. Yeye ni mushuhuda mwaminifu, naye ndiye wa kwanza aliyefufuliwa, vilevile yeye ni mukubwa wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametukomboa toka katika zambi zetu kwa njia ya damu yake.


Ninyi watumwa, mutii wabwana wenu kwa woga na kutetemeka na kwa moyo wa ukweli kama vile munavyomutumikia Kristo.


Wewe hauna sehemu wala haki yoyote katika jambo hili, kwa sababu moyo wako si mukamilifu mbele ya Mungu.


Wakati waliposikia maneno haya, wakaondoka wote mumoja kwa mumoja, wakianzia kwa wazee. Yesu akabaki pale peke yake pamoja na yule mwanamuke aliyekuwa akisimama mbele yake.


Moyo wangu ukuwe mukamilifu juu ya masharti yako, kusudi nisifezeheke.


Wenye kiburi wanasema uongo juu yangu, lakini mimi ninashika kanuni zako kwa moyo wote.


Ninataka kukupendeza kwa moyo wangu wote; unionee huruma kama ulivyoahidi!


Unieleweshe nipate kushika sheria yako, niifuate kwa moyo wangu wote.


Ninakutafuta kwa moyo wote; usiniachilie kugeuka mbali na amri zako.


Heri wanaoshika maagizo yake, wanaomutafuta kwa moyo wao wote,


Haleluia! Nitamushukuru Yawe kwa moyo wangu wote, katika mukutano wa watu wa usawa.


Maana hukumu zitatolewa kwa haki tena, na wote wenye moyo wa usawa watazifuata.


Siku moja tu ndani ya hekalu lako, ni bora kuliko siku elfu pahali pengine; afazali kubakia kwa mulango wa nyumba yako, kuliko kuishi ndani ya nyumba ya waovu.


Mufurahi na kushangilia kwa sababu ya Yawe, enyi watu wa haki; mupige vigelegele vya shangwe, enyi wenye moyo wa usawa.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo “Kilio cha mwana.”


Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe unapima moyo, nawe unapendezwa na uaminifu. Nami, katika uaminifu wa moyo wangu nimetoa vitu hivi vyote kwa mapenzi yangu, na sasa ninaona watu wako wanaokuwa hapa, wakikutolea kwa mapenzi yao na furaha.


Kutoka kabila la Isakari: wakubwa mia mbili pamoja na wandugu zao wote waliokuwa chini ya waangozi wao. Wakubwa hao walikuwa na elimu ya kujua mambo ya nyakati na walijua mambo Waisraeli waliyopasha kufanya.


Abiyamu alitenda zambi zilezile baba yake alizotenda, wala hakukuwa na moyo mwaminifu kwa Yawe, Mungu wake, kama babu yake Daudi alivyokuwa.


Ataoga mwili wote katika maji, kisha atavaa nguo takatifu. Ataingia pahali pale akiwa amevaa nguo takatifu: koti la kitani na atavaa kapitula ya kitani na akiwa amevaa kanzu ya kitani na kujifunga mukaba wa kitani.


Muheshimiwa Teofilo: Watu wengi wamejaribu kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka katikati yetu. Wameyaandika sawa vile tulivyoelezwa na wale walioona mambo yale tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe ule. Inafaa nami vilevile kisha kuchunguza kwa uangalifu mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa utaratibu,


Basi sasa, unangojea nini? Simama ubatizwe na kuondolewa zambi zako, ukiomba kwa jina la Bwana.’ ”


Lakini tunatamani sana kwamba kila mumoja kati yenu aendelee kuonyesha bidii ile mpaka mwisho, kusudi mambo yale munayotumainia yapate kutimizwa.


Sheria ya Kiyuda ni mufano wa mema yatakayotokea, lakini si kitambulisho kinachoonyesha mambo yale kamili. Kwa sababu hii Sheria haiwezi hata mara moja, kwa njia ya sadaka zinazotolewa mara nyingi kila mwaka, kuwafanya wakamilifu wale wanaomwendea Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite