Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 8:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Malaika wa kwanza akapiga baragumu. Halafu mvua ya mawe na moto vyenye kuchanganyika na damu, vikatupwa katika dunia. Sehemu moja ya tatu ya inchi ikateketea, na sehemu moja ya tatu ya miti na majani yote vikateketea vilevile.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 8:7
29 Referans Kwoze  

Wakaambiwa wasiharibu majani yoyote wala mumea wowote, wala muti wowote, lakini wawatese watu wasiokuwa na chapa ya muhuri wa Mungu kwenye paji za nyuso zao.


Nitamwazibu Gogi kwa ugonjwa mukali na mauaji. Nitanyesha mvua nyingi na mvua ya mawe na moto na kiberiti juu yake, juu ya makundi yake, na mataifa yale mengi yanayokuwa pamoja naye.


Na sehemu moja ya tatu ya wanadamu wakauawa kwa mapigo hayo matatu: kwa moto, moshi na viberiti vilivyotoka ndani ya vinywa vya wale farasi,


Wale wamalaika wane wakafunguliwa, nao walikuwa wamewekwa tayari kwa saa ile, siku, mwezi na mwaka ule, wapate kuua sehemu moja ya tatu ya wanadamu.


Bwana amejichagulia mutu wake shujaa na mwenye nguvu, ambaye ni kama mvua ya mawe na zoruba kali, kama zoruba ya mafuriko makubwa; kwa mukono wake atawatupa chini.


Kwa pahali pa mvua akawatumia mvua ya mawe, na radi iliyounguza inchi yao yote;


Kisha mvua ya mawe makubwa yenye uzito wa zaidi ya kilo makumi ine ikanyesha juu ya watu. Nao wakamutukana Mungu kwa sababu ya hilo pigo la mvua ya mawe, kwa maana pigo lile lilileta hasara kubwa sana.


Lakini mvua ya mawe itanyesha na kuangusha pori, na muji wake utaangamizwa.


Yawe atawafanya watu wote waisikie sauti yake tukufu na pigo la nguvu yake lionekane kwa hasira nyingi. Kutakuwa ndimi za moto mukali, ngurumo, zoruba na mvua ya mawe.


Yawe wa majeshi atakuja kukusaidia; atakuja na ngurumo, tetemeko la inchi na sauti kubwa; atakuja na upepo mukali, zoruba na moto wenye kuunguza.


Walipokuwa wakiwakimbia Waisraeli kwenye muteremuko wa Beti-Horoni, Yawe akawanyeshea mvua ya mawe makubwa kutoka mbinguni wakiwa katika njia mpaka Azeka hata waliouawa kwa mawe hayo wakakuwa wengi kuliko waliouawa kwa silaha za Waisraeli.


Malaika wa kwanza akamwanga kikombe chake katika dunia. Halafu majipu mabaya na yenye kuumiza sana yakaota juu ya watu waliokuwa na chapa ya yule nyama na walioabudu sanamu yake.


Mukia wake ulikokota sehemu moja ya tatu ya nyota za mbingu na kuzitupa katika dunia. Yule nyoka akasimama mbele ya yule mwanamuke aliyekuwa tayari kuzaa, kusudi amumeze mutoto wakati atakapozaliwa.


Nikaangalia, nami nikaona farasi mwenye rangi ya kijivujivu. Na yule aliyepanda juu yake aliitwa Lufu, naye alikuwa akisindikizwa na Kuzimu. Wao wakapewa uwezo juu ya sehemu moja ya ine ya dunia kwa kuua watu kwa upanga, kwa njaa kubwa, kwa ugonjwa mukali na kwa nyama wakali.


Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Wanadamu wote ni kama majani. Na utukufu wao wote unatoweka kama maua. Majani yanakauka na maua yanaanguka.


Jua linatokea na kwa joto kali linakausha mimea, nayo maua yake yanaanguka na uzuri wake wote unaharibika. Hivi ndivyo tajiri naye atakavyotoweka katika shuguli zake.


Basi, Musa akaondoka katika nyumba ya mufalme, akatoka inje ya muji. Kisha akainua mikono yake kumwomba Yawe. Ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua ikaacha kunyesha katika dunia.


Kisha mambo yale, nikaona wamalaika wane wakisimama kwenye pembe ine za dunia, wakizuiza upepo toka pande ine za dunia, kusudi usivume juu ya dunia, wala juu ya bahari, wala juu ya muti wowote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite