Ufunuo 8:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
11 (Jina la ile nyota ni Uchungu.) Basi sehemu moja ya tatu ya maji ikakuwa uchungu, na watu wengi waliokunywa maji yale walikufa kwa sababu ya sumu iliyokuwa ndani yake.
Kwa hiyo, Yawe wa majeshi anasema hivi juu ya manabii wa Yerusalema: Nitawakulisha uchungu, na kuwapa maji yenye sumu wakunywe. Maana kutoka kwa manabii wa Yerusalema kutomwogopa Mungu kumeenea kila pahali katika inchi.
Nitawatawanya kati ya mataifa ambayo wao wenyewe wala babu zao hawakupata kuyajua; na kisha nitatuma vita nyuma yao mpaka hapo nitakapowaangamiza wote.
Kisha kusikia maneno ya agano hili ambayo mumeapishwa, na mutu akijiamini mwenyewe ndani ya moyo wake na kusema atakuwa salama naye akifuata ugumu wake, hiyo italeta maangamizi.
Farasi wanaweza kukimbia katika mawe makubwa? Watu wanaweza kulima bahari na ngombe? Lakini ninyi mumeigeuza sheria kuwa sumu, na tunda la haki kuwa uchungu.
Malaika wa kwanza akapiga baragumu. Halafu mvua ya mawe na moto vyenye kuchanganyika na damu, vikatupwa katika dunia. Sehemu moja ya tatu ya inchi ikateketea, na sehemu moja ya tatu ya miti na majani yote vikateketea vilevile.
Muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asijikoseshe mwenyewe kupata neema ya Mungu, wala asikuwe sawa shina la mumea unaotoa matunda machungu na kuleta fujo kati yenu na kuambukiza watu wengi.
Walipofika pahali panapoitwa Mara, hawakuweza kunywa maji ya Mara kwa sababu yalikuwa machungu. Kwa sababu hiyo pahali pale pakaitwa Mara, ni kusema “Uchungu”.
Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.
Mukia wake ulikokota sehemu moja ya tatu ya nyota za mbingu na kuzitupa katika dunia. Yule nyoka akasimama mbele ya yule mwanamuke aliyekuwa tayari kuzaa, kusudi amumeze mutoto wakati atakapozaliwa.