Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 8:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Wakati Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa saba, kukakuwa kimya mbinguni kwa muda wa nusu ya saa.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 8:1
14 Referans Kwoze  

Kweli, nitawashambulia wale waliowakamata mateka, nao watakamatwa mateka na wale waliowafanya watumwa wao. Halafu kwa hiyo mutajua kwamba Yawe wa majeshi ndiye aliyenituma.


Lakini Yawe yuko katika hekalu lake takatifu; dunia yote ikae kimya mbele yake.


Kisha nikaona mambo haya: Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa kwanza kati ya ile mihuri saba, nikasikia kimoja kati ya vile viumbe vya ajabu kikisema hivi kwa sauti kama ya ngurumo ya radi: “Kuja!”


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa Yedutuni. Zaburi ya Daudi.


Kitu kimoja kikasimama mbele yangu. Nilipokiangalia sikukitambua kabisa. Kulikuwa umbo moja mbele yangu. Kulikuwa kimya, kisha nikasikia sauti:


Kisha nikaona mambo haya: Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa sita, kukakuwa tetemeko kubwa la dunia; jua ikageuka kuwa nyeusi kama nguo ya kilio na mwezi ukageuka kuwa mwekundu kama damu.


Wakati Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa tano, nikaona chini ya mazabahu, roho za watu waliouawa kwa sababu ya kutangaza Neno la Mungu na kwa sababu ya ushuhuda wao.


Kisha nikaona kizingo cha karatasi katika mukono wa kuume wa yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme. Kizingo kile kilikuwa kimeandikwa ngambo na ngambo na kufungwa kwa vifundo saba vya mihuri.


Wakati Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa ine, nikasikia sauti ya kiumbe cha ine cha ajabu kikisema: “Kuja!”


Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa tatu, nikasikia kiumbe cha tatu cha ajabu kikisema: “Kuja!” Niliangalia nami nikaona farasi mweusi. Na yule aliyepanda juu yake alikuwa na mizani katika mikono yake.


Kisha Mwana-Kondoo akafungua kifundo cha muhuri wa pili. Nikasikia kiumbe cha pili cha ajabu kikisema: “Kuja!”


Tulia mbele ya Yawe, umungojee kwa uvumilivu; usihangaike juu ya wale wanaofanikiwa, ndio watu wanaojaliwa katika mipango yao mibaya.


Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.


Basi wakaenda, wakatia muhuri juu ya lile jiwe, na wakaweka waaskari pale kwa kulichunga.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite