Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 7:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kisha mambo haya, nikaangalia nami nikaona mukutano mukubwa sana wa watu wasioweza kuhesabiwa. Kulikuwa watu wa kila taifa, wa kila kabila, wa kila jamaa na wa kila luga. Walikuwa wakisimama mbele ya kiti cha kifalme na mbele ya Mwana-Kondoo, wakivaa kanzu nyeupe na kushika matawi ya muti wa ngazi katika mikono yao.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 7:9
41 Referans Kwoze  

Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.


Basi wakatwaa matawi ya ngazi na kwenda kumupokea, wakilalamika kwa sauti kubwa, wakisema: “Mungu asifiwe! Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana! Abarikiwe mufalme wa Waisraeli!”


Uniombe nami nitakupa mataifa kuwa urizi wako, na dunia nzima kuwa mali yako.


Haraka! Ninyi wote munaokaa katika inchi ya Babeli, mukimbilie Sayuni!


Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


Kila mumoja wao akapewa kanzu nyeupe, wakaambiwa wapumzike kwa muda kidogo mpaka wakati hesabu ya watumishi wenzao na wandugu watakaouawa vilevile kama wao itakapotimia.


Kwa hiyo ninakushauria kununua kwangu zahabu iliyosafishwa kwa moto, kusudi upate kuwa tajiri. Vilevile ununue nguo nyeupe, upate kuvaa na kufunika uchi wako unaokuletea haya. Tena ununue dawa ya kutia ndani ya macho yako, kusudi upate kuona.


Wandugu zangu, sitaki mukose kujua siri hii, kusudi musijione kuwa wenye akili sana. Siri ile ni hii: Waisraeli wamoja wataendelea kuwa wagumu mpaka watu wa mataifa mengine kwa jumla watakapokuja kwa Mungu.


Wakati huo, Yerusalema utaitwa “Kiti cha Kifalme cha Yawe”, na mataifa yote yatakusanyika humo mbele yangu. Hawatafuata tena ugumu wao unaotokana na matendo yao mabaya.


Basi mukeshe na kuomba kila wakati, kusudi mupate nguvu ya kuepuka mambo hayo yote yatakayotokea, nanyi mupate kuweza kusimama mbele ya Mwana wa Mutu.”


Wakati ule ule makundi mengi ya maelfu ya watu walikusanyika hata wakakanyaganakanyagana. Yesu akaanza kwanza kusema na wanafunzi wake, akiwaambia: “Mufanye angalisho na chachu ya Wafarisayo, maana yake unafiki wao.


Wamasikini watakula na kushiba; wanaomutafuta Yawe watamusifu. Mungu awajalie waishi milele!


Katika siku ya kwanza mutatwaa matunda ya miti yenu mizuri, matawi ya ngazi, matawi yenye majani mengi na matawi ya miti inayoota kandokando ya muto, nanyi mutafanya sikukuu mbele ya Yawe, Mungu wenu kwa siku saba.


Na kiti kile kilikuwa kimezungukwa na viti vingine makumi mbili na vine vya kifalme na juu ya viti vile kulikuwa kumeikaa wazee makumi mbili na wane. Wale wazee walikuwa wamevaa nguo nyeupe na juu ya kichwa chao kulikuwa taji za zahabu.


Lakini ninyi mumefikia kwenye mulima Sayuni na kwenye muji wa Mungu Mwenye Uzima, ndio muji Yerusalema wa mbinguni, kunakokuwa maelfu na maelfu ya wamalaika.


Kwa sababu hiyo, kwa njia ya mutu mumoja aliyekuwa akingojea kufa, kukazaliwa wazao wengi sana kama nyota na kama muchanga unaokuwa kandokando ya bahari.


Kwa hiyo sasa mutwae silaha zote Mungu anazowapatia. Kwa njia hii mutaweza kushinda adui yenu siku mbaya itakapowafikia. Nanyi mutakapokwisha kumaliza mapigano, mutaweza kusimama imara.


Mufalme akaamuru wale watu waliomuchongea Danieli wakamatwe, nao wakatupwa ndani ya lile pango la simba pamoja na wake wao na watoto wao. Nao, hata mbele hawajagusa chini, simba waliwashambulia na kuivunjavunja mifupa yao.


Amekumbuka wema na uaminifu wake kwa Waisraeli. Pande zote za dunia zimeuona ushindi wa Mungu wetu.


Mimi, Nebukadneza, nilikuwa ninaishi katika raha na amani katika nyumba yangu ya kifalme.


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


Kisha nikaangalia tena, nikasikia sauti ya wamalaika wengi wenye kuzunguka kiti cha kifalme, na viumbe vya ajabu na wazee. Hesabu yao ilikuwa maelfu na maelfu na mamilioni na mamilioni.


Ninamulilia Mungu kwa sauti. Kwa sauti ninamulilia Mungu, anisikie.


Wazao wako nitawafanya wakuwe wengi wasihesabike, kama vile mavumbi ya inchi. Kama vile vumbi isivyoweza kuhesabika, ndivyo wazao wako hawataweza kuhesabika!


Ee Yawe! Wewe ndiwe nguvu yangu na upango wangu; wewe ni kimbilio langu wakati wa taabu. Mataifa toka pande zote za dunia yatakufikia na kusema: Miungu ya babu zetu ilikuwa ya uongo, ilikuwa ya bure, isiyofaa kitu.


Kule alivunja mishale ya waadui; alivunja ngao, panga na silaha za vita.


Nitawaita watu wangu na kuwakusanya pamoja; nimekusudia kuwakomboa, nao watakuwa wengi kama vile mbele.


Hakutakuwa tena kitu chochote kinacholaaniwa na Mungu. Kiti cha kifalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwa ndani ya muji ule, na watumishi wa Mungu watamwabudu.


Akapima metre mia tano zingine, na muto ukakuwa na kilindi kirefu hata sikuweza kuuvuka tena. Haikuwezekana kuuvuka lakini kwa kuogelea.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite