Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 7:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 “Musiharibu dunia, wala bahari, wala miti mpaka tutakapokwisha kutia chapa ya muhuri juu ya paji ya nyuso za watumishi wa Mungu wetu.”

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 7:3
31 Referans Kwoze  

Wataona uso wake na jina lake litaandikwa juu ya paji za nyuso zao.


akamwambia hivi: Pita katikati ya Yerusalema, upate kutia kitambulisho kwenye vipaji vya nyuso za watu wanaohuzunika na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika muji huu.


Wakaambiwa wasiharibu majani yoyote wala mumea wowote, wala muti wowote, lakini wawatese watu wasiokuwa na chapa ya muhuri wa Mungu kwenye paji za nyuso zao.


Kisha nikaona viti vya kifalme na watu waliokuwa wakiikaa juu yao, wakapewa uwezo wa kuhukumu. Nikaona vilevile roho za wale waliochinjwa kwa sababu ya kutangaza ukweli ulioshuhudiwa na Yesu na Neno la Mungu. Watu wale hawakumwabudu yule nyama wa ajabu, wala sanamu yake, wala hawakupigwa chapa yake juu ya paji za nyuso zao, au juu ya mikono yao. Nao wakafufuka na kutawala pamoja na Kristo muda wa miaka elfu moja.


Kisha nikaangalia, nikaona Mwana-Kondoo akisimama juu ya mulima Sayuni. Naye alikuwa pamoja na watu elfu mia moja makumi ine na ine, na juu ya paji za nyuso za watu wale kulikuwa kumeandikwa jina lake na jina la Baba yake.


Na yule nyama akawalazimisha watu wote, wadogo na wakubwa, watajiri na wamasikini, wanaokuwa huru na watumwa, wapigwe chapa juu ya mikono yao ya kuume na juu ya paji za nyuso zao.


Basi, ile damu itakuwa kitambulisho chenu cha kuonyesha nyumba mutakamokuwa. Nami nitakapoiona ile damu, nitawapita ninyi, hamutapatwa na hasara yoyote wakati nitakapoipiga inchi ya Misri.


Silaha zote zilizotengenezwa kwa kukuzuru wewe hazitafaa kwa kitu chochote. Mutu akikushitaki, utamushinda. Hiyo ndiyo haki niliyowapangia watumishi wangu. Hizo ndizo haki nilizowahakikishia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Hukumu zake ni za kweli na za haki. Amehukumu yule kahaba mukubwa ambaye alikuwa akipotosha dunia kwa vitendo vyake vya uasherati. Mungu amemulipiza kisasi cha damu ya watumishi wake!”


Nikasikia kitu kama sauti iliyotokea katikati ya vile viumbe vine vya ajabu ikisema: “Kilo moja ya ngano ni mushahara wa siku nzima ya kazi, na kilo tatu ya shayiri ni mushahara wa siku nzima ya kazi, lakini usiharibu mafuta wala divai.”


Pale ndipo mutakapotambua tena tofauti inayokuwa kati ya wenye haki na waovu, kati ya mutu anayemutumikia Mungu na asiyemutumikia.


Maana Yawe atapita kuwaua Wamisri. Lakini atakapoona damu iliyopakwa kwenye vizingiti na miimo ya nyumba zenu, atapita na wala hatamuruhusu mwangamizaji kuingia katika nyumba zenu na kuwaua.


Kama mutu akitaka kunitumikia, anapaswa kunifuata, na hivi mutumishi wangu atakuwa popote nitakapokuwa. Mutu akinitumikia, Baba yangu atamupa heshima.


Na kama Mungu asingepunguza siku zile za mateso, hakuna hata mutu mumoja angeponyoka kufa. Lakini kwa ajili ya watu wake aliowachagua, yeye atazipunguza.


Mutafute Yawe, enyi wanyenyekevu wote katika inchi, enyi munaozitii amri zake. Mutafute haki, mutafute unyenyekevu; labda mutaiponyoka siku ya kasirani ya Yawe.


Yawe anasema hivi: Mutu akikuta kishada cha mizabibu mizuri, watu wanasema: Tusikiharibu; kina baraka. Ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.


Aliwaazibu watu wake kwa kuwapeleka katika uhamisho. Wakati wa upepo mukali wa mashariki, aliwaondoa kwa pigo kali.


Hata kukibaki sehemu moja ya kumi ya watu, nao vilevile watateketezwa. Hao watakuwa kama muti wa muvinje au wa mwalo ambao shina lake limebaki kisha kukatwa. Shina hilo ni mbegu takatifu ya mwanzo mupya.


Lakini sasa kufuatana na vile mumewekwa huru toka utawala wa zambi na kugeuka watumwa wa Mungu, munapata faida ya kuishi katika utakatifu na kwa mwisho kupewa uzima wa milele.


Baragumu kubwa itapigwa, halafu atawatuma wamalaika wake katika pande ine za dunia, kusudi wawakusanye watu wake aliowachagua, kutoka katika dunia nzima.


Wale watu kwa pamoja wakamwendea mufalme Dario na kumwambia: Ee mufalme, ujue kwamba hakuna sheria wala amri yoyote ya Wamedi na Wapersi inayoweza kubadilishwa kisha kuwekwa na mufalme.


Basi, mufalme Nebukadneza akaukaribia mulango wa furu la moto mukali, akaita: Sadiraki, Mesaki na Abedenego, watumishi wa Mungu Mukubwa, mutoke mukuje hapa! Sadiraki, Mesaki na Abedenego wakatoka ndani ya moto.


Mungu wetu ambaye tunamutumikia anaweza kutuokoa. Atatuokoa kutoka furu la moto mukali na vilevile kutoka katika mikono yako, ee mufalme.


Muwaue wazee palepale, vijana wanaume na wabinti, watoto na wanawake; lakini kila mumoja mwenye kuwa na kitambulisho, musimuguse. Muanzie katika hekalu langu. Basi, wakaanza na wazee waliokuwa mbele ya nyumba ya Yawe.


Yeyote anayekubali ushuhuda wake anahakikisha kama Mungu ni mwenye ukweli.


Kisha mambo yale, nikaona wamalaika wane wakisimama kwenye pembe ine za dunia, wakizuiza upepo toka pande ine za dunia, kusudi usivume juu ya dunia, wala juu ya bahari, wala juu ya muti wowote.


Nikaona malaika mwingine akipanda tokea mashariki alikuwa akishika muhuri wa Mungu Mwenye Uzima. Akawalalamikia kwa sauti kubwa wale wamalaika wane waliopewa uwezo wa kuharibu dunia na bahari:


Na hakukukuwa mutu aliyeweza kununua wala kuuzisha kitu pasipo kuwa na chapa ya jina la nyama yule au tarakimu zinazolingana na herufi za jina lile.


Na malaika wa tatu akafuata wale wawili wa kwanza, akisema kwa sauti kubwa: “Kila mutu anayeabudu yule nyama na sanamu yake na kupigwa chapa juu ya paji la uso wake au juu ya mukono wake,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite