Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 7:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Nao hawatasikia njaa tena, wala kiu, wala jua halitawapiga tena, wala joto lolote.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 7:16
23 Referans Kwoze  

Hawatasikia tena njaa wala kuwa na kiu. Upepo wenye kuunguza wala jua havitawachoma, mimi niliyewahurumia nitawaongoza na kuwapeleka kwenye chemichemi za maji.


lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”


Yeye atapanguza machozi yao yote na kifo hakitakuwa tena, wala kilio, wala malalamiko, wala maumivu. Kwa maana dunia ya mbele imekwisha kupita.”


Heri wale wanaokuwa na njaa na kiu ya kufanya yanayokuwa haki, maana watashibishwa!


Muchana jua halitakuchoma, wala mwezi hautakuzuru usiku.


Heri kwenu munaokuwa wenye njaa sasa, maana mutashibishwa. Heri kwenu munaolia sasa, maana mutacheka.


Anawatajirisha wenye njaa, lakini amewaacha watajiri mikono mitupu.


Wamasikini na wakosefu wakitafuta maji lakini hawayapati, wakiwa wamekauka koo kwa kiu, mimi Yawe nitawajibu; mimi Mungu wa Israeli, sitawaacha.


Maana wewe umekuwa kimbilio kwa wazaifu, pango kwa wakosefu katika taabu zao. Wewe ni kimbilio wakati wa zoruba, kivuli wakati wa joto kali. Kweli pigo la watu wakali ni kali kama zoruba inayopiga ukuta;


Basi, mimi Yawe ninasema: Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mutasikia njaa; watumishi wangu watakunywa, lakini ninyi mutasikia kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mutafezeheka.


Wakati jua lilipokuwa kali, likazichoma, na kwa sababu hazikukuwa na mizizi mikubwa, zikakauka.


Musinishangae kwa sababu mimi ni mweusi. Ni kwa sababu jua limenichoma. Wandugu zangu walinikasirikia, wakanifanya kuwa mutumishi katika mashamba ya mizabibu. Lakini sikuchunga shamba langu la mizabibu.


Kama pongo anavyotamani maji ya kijito, ndivyo ninavyokutamani, ee Mungu wangu!


Jua linatokea na kwa joto kali linakausha mimea, nayo maua yake yanaanguka na uzuri wake wote unaharibika. Hivi ndivyo tajiri naye atakavyotoweka katika shuguli zake.


Lakini halizami ndani yao kama mizizi; wanalishika kwa muda mufupi tu. Wakati taabu na mateso vinapowafikia kwa ajili ya Neno la Mungu, mara moja wanaanguka.


Wakati jua lilipokuwa kali, likazichoma, na kwa sababu hazikukuwa na mizizi mikubwa zikakauka.


Lakini halizami ndani yao kama mizizi. Wanalishika kwa muda mufupi tu. Wakati taabu na mateso vinapowafikia kwa ajili ya Neno la Mungu, mara moja, wanaanguka.


Jua lilipotokea, Mungu akaleta upepo mukali kutoka upande wa jangwa, jua likamuchoma sana Yona juu ya kichwa, karibu azimie. Akatamani kufa, akisema: Ni vizuri kwangu kufa kuliko kuishi.


Kila mumoja atakuwa kama pahali pa kujikinga na upepo, kama pahali pa kujificha wakati wa mvua kubwa. Watakuwa kama vijito vya maji katika inchi yenye kukauka, kama kivuli cha jiwe kubwa katika jangwa.


Ninakunyooshea mikono yangu. Ninakuhitaji wewe, kama inchi kavu inavyohitaji mvua.


Zaburi ya Daudi wakati alipokuwa katika jangwa la Yudea.


Yawe ni mulinzi wako; yuko upande wako wa kuume kwa kukukinga.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite