Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 7:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 wakisema: “Amina! Utukufu, sifa, hekima, shukrani, heshima, uwezo, na nguvu ni vya Mungu wetu, milele na milele! Amina!”

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 7:12
27 Referans Kwoze  

yeye anayekuwa Mungu peke yake, Mwokozi wetu, asifiwe na kuwa na ukubwa, uwezo na mamlaka, kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu, tangia zamani za kale, sasa na hata milele! Amina.


Na wale wazee makumi mbili na wane na vile viumbe vine vya ajabu wakainama chini na kumwabudu Mungu, anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakisema: “Amina! Mungu asifiwe!”


Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.


Muingie ndani ya hekalu lake kwa shukrani, muingie katika kiwanja chake kwa kumusifu. Mumushukuru na kulisifu jina lake.


Watu wanaoabudu sanamu za miungu ya bure, wanautupilia mbali uaminifu wao kwako.


Mumwimbie Yawe nyimbo za shukrani, mumupigie Mungu wetu kinubi!


Wamutolee sadaka za shukrani; waeleze matendo yake kwa nyimbo za shangwe.


Ee Yawe, ona jinsi wanavyomuzomea muchaguliwa wako. Wanamuzomea kila fasi anapokwenda.


Jina lake tukufu litukuzwe milele; utukufu wake ujae katika ulimwengu wote! Amina, Amina!


Wewe unaniimarisha katika ukamilifu; utanichunga mbele yako milele.


sauti za arusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wanaleta sadaka za shukrani katika nyumba ya Yawe. Wataimba hivi: Mumushukuru Yawe wa majeshi kwa sababu Yawe ni muzuri, kwa maana wema wake unadumu milele. Nitairudishia inchi hii hali yake ya zamani. –Ni Yawe anayesema.


Mimi Yawe nitaufariji Sayuni, nitatengeneza pahali pake pote palipoharibika. Nitazifanya mbuga zake kama shamba la Edeni, jangwa yake kama bustani ya Yawe. Ndani yake kutapatikana furaha na shangwe, na nyimbo za shukrani zitasikilika humo.


Mukuwe na mizizi ndani yake, mujijenge juu yake na kusimama imara katika imani sawa vile mulivyofundishwa. Na zaidi ya hii mukuwe wenye kushukuru sana.


Kwa maana mambo haya yote yanafika kwa ajili yenu kusudi neema ya Mungu izidishwe kwa watu wengi siku zote, nao wapate kumutolea Mungu shukrani nyingi kwa ajili ya utukufu wake.


Nitakutolea sadaka za shukrani. Nitaomba kwa jina la Yawe.


Yawe, Mungu wa Israeli, asifiwe tangu milele na hata milele! Na watu wote waseme: “Amina!” Haleluia!


Tuende mbele yake na nyimbo za shukrani; tumushangilie kwa nyimbo za sifa.


Usituache kuanguka katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. [Kwa maana ufalme, uwezo na utukufu ni vyako hata milele. Amina.]’


Nao muji huu utakuwa kwangu jina la furaha, sifa na utukufu mbele ya mataifa yote katika dunia ambayo yatasikia juu ya mema yote ninayowafanyia. Mataifa yataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mema na amani nitakazouletea muji huu wa Yerusalema.


Shukrani ikuwe ndiyo sadaka yako kwa Mungu. Umutimizie Mungu Mukubwa ahadi zako.


Tangu wakati wa mufalme Daudi na Asafu kulikuwa kiongozi wa waimbaji, na kulikuwa nyimbo za sifa na shukrani kwa Mungu.


Walawi walikuwa: Yesua, Binui, Kadimieli, Serebia, Yuda na Matania, ambaye alishugulika na usimamizi wa nyimbo za shukrani akishirikiana na ndugu zake.


Mimi ni mwenye uzima. Nilikuwa nimekufa, lakini sasa mimi niko muzima kwa milele na milele. Niko na mamlaka juu ya lufu na kuzimu.


Kwa maana vitu vyote vinatoka kwake, navyo viko kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Atukuzwe hata milele! Amina.


Kwa maana kama ukimwomba Mungu ndani ya roho tu kwa kumushukuru, mutu asiyeelewa kitu anayehuzuria katika mukutano hawezi kusema amina kwa kuitikia maombi yako ya kushukuru. Ni kwa sababu hasikii mambo unayosema.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite