Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 7:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Nao walilalamika hivi kwa sauti kubwa: “Wokovu wetu unatoka kwa Mungu wetu anayeikaa juu ya kiti cha kifalme na kwa Mwana-Kondoo!”

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 7:10
26 Referans Kwoze  

Kisha mambo hayo, nikasikia kelele kutoka mbinguni linalosikilika kama vile sauti kubwa ya kundi kubwa la watu ikisema: “Mungu asifiwe! Wokovu, utukufu na uwezo ni vya Mungu wetu. Yeye anastahili utukufu na uwezo.


Ee Yawe, ee Mungu wangu, wewe unayevunja waadui zangu wote mataya, unayeponda waovu meno, simama sasa uniokoe!


Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni, ikisema: “Sasa wokovu, uwezo na ufalme wa Mungu, na mamlaka ya Kristo wake vimefika. Ni vile, kwa yule aliyekuwa akiwashitaki wandugu zetu mbele ya Mungu wetu muchana na usiku ametupwa chini ya mbingu.


Mutangaze na kusema habari zenu. Mufanye shauri pamoja! Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa? Ni nani aliyesema mambo haya zamani? Haikukuwa mimi Yawe? Hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi! Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi; hakuna mwingine isipokuwa mimi.


Hakutakuwa tena kitu chochote kinacholaaniwa na Mungu. Kiti cha kifalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwa ndani ya muji ule, na watumishi wa Mungu watamwabudu.


Kwa maana mumeokolewa kwa neema ya Mungu, kwa njia ya imani. Jambo hili halitokani na ninyi wenyewe, lakini ni zawadi ya Mungu.


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Mimi peke yangu ndiye Yawe, hakuna mukombozi mwingine isipokuwa mimi.


Basi yule aliyekuwa akiikaa juu ya kiti cha kifalme akasema: “Angalia ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Kisha akaniambia: “Andika maneno haya, kwa maana ni ya kweli na ya uhakika.”


Kila mutu ataona jinsi Mungu atakavyotuokoa.’ ”


Kweli tumedanganyika sana kwa kutambikia huko kwenye vilima, hakika wokovu wa Israeli unatoka kwake Yawe, Mungu wetu.


Yule Mwana-Kondoo akajongea na kukamata kizingo kutoka mukono wa kuume wa yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme.


Tena mbele ya kiti kile kulionekana kama bahari ya kioo, kulingaa sana kama kilauri. Kile kiti cha kifalme kilikuwa kimezungukwa pande zote na viumbe vine vya ajabu, vyenye kujaa macho mbele na nyuma.


Ninyi Wasamaria hamujui munachokiabudu; sisi tunajua tunachokiabudu kwa sababu wokovu unatokea kwa njia ya Wayuda.


Wakati alipomwona Yesu akipita, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu.”


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Watu wanaoabudu sanamu za miungu ya bure, wanautupilia mbali uaminifu wao kwako.


Yawe anasema: Lakini mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri; hakuna mungu mwingine lakini mimi, wala hakuna anayeweza kuwaokoa.


Kweli wewe ni Mungu mwenye kufichama, Mungu wa Israeli, Mungu mwokozi.


Si sisi, ee Yawe, si sisi; lakini wewe peke yako utukuzwe, kwa ajili ya wema na uaminifu wako.


Yawe anawaokoa watu wa haki, na kuwalinda wakati wa taabu.


Tena, akaongeza kusema: Mulima huu ni kizuizi? Hapana! Wewe Zerubabeli utausawazisha. Wewe utaanzisha ujenzi mupya wa hekalu, na wakati utakapoliweka jiwe la mwisho, watu watashangilia wakisema: Ni zuri! Kweli, ni zuri!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite