Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 5:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Wakati alipokuwa amekwisha kukamata kizingo, vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee makumi mbili na wane wakainama uso mpaka chini mbele ya Mwana-Kondoo. Kila mumoja wao alikuwa na kinubi na vikombe vya zahabu vilivyojaa marasi, ndiyo maombi ya watu wa Mungu.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 5:8
27 Referans Kwoze  

Upokee maombi yangu kama ubani; ninapoinua mikono yangu kwako, unikubali kama sadaka ya magaribi.


wale wazee makumi mbili na wane waliinama uso mpaka chini mbele ya yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakimwabudu huyo anayeishi kwa milele na milele. Nao walikuwa wakikuja kuweka taji zao mbele ya kiti chake, na kusema:


Vile viumbe vine vya ajabu vilijibu: “Amina.” Na wale wazee wakainama uso mpaka chini na kuabudu.


Na kiti kile kilikuwa kimezungukwa na viti vingine makumi mbili na vine vya kifalme na juu ya viti vile kulikuwa kumeikaa wazee makumi mbili na wane. Wale wazee walikuwa wamevaa nguo nyeupe na juu ya kichwa chao kulikuwa taji za zahabu.


Na wale wazee makumi mbili na wane na vile viumbe vine vya ajabu wakainama chini na kumwabudu Mungu, anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakisema: “Amina! Mungu asifiwe!”


Halafu nikaona Mwana-Kondoo akisimama katikati ya kiti cha kifalme chenye kuzungukwa na vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee, naye alionekana kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba; ndizo roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote.


Na kila kimoja cha viumbe vya ajabu kilikuwa na mabawa sita yenye kujaa macho ndani na inje. Navyo viliimba muchana na usiku bila kuchoka, vikisema: “Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, aliyekuwa, anayekuwa na anayekuja.”


Mumusifu Yawe kwa zeze; mumwimbie kwa kinubi cha nyuzi kumi.


Na mumoja wa vile viumbe vine vya ajabu akawapa wale wamalaika saba vikombe saba vya zahabu vyenye kujaa kasirani ya Mungu, anayeishi kwa milele.


Tena nikaona kitu kinachofanana na bahari ya kioo, iliyochanganyika na moto. Nikaona vilevile wale walioshinda yule nyama wa ajabu pamoja na sanamu yake na tarakimu zinazolingana na herufi za jina lake. Watu wale walikuwa wakisimama juu ya ile bahari ya kioo wakishika vinubi walivyopewa na Mungu.


kusudi watu wote wamuheshimu Mwana kama vile wanavyomuheshimu Baba. Asiyemuheshimu Mwana, hamuheshimu Baba aliyemutuma.


Mumwimbie Mungu kwa sauti, maana ni nguvu yetu, mumushangilie Mungu wa Yakobo,


Hapo, ee Mungu, nitakwenda kwenye mazabahu yako; nitakuja kwako, ee Mungu, wewe furaha yangu kubwa. Nitakusifu kwa zeze, ee Mungu, Mungu wangu.


Mumusifu kwa mulio wa baragumu, mumusifu kwa zeze na kinubi!


Na tena wakati Mungu alipomutuma muzaliwa wake wa kwanza katika dunia, alisema: “Wamalaika wote wa Mungu wanapaswa kumwabudu.”


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Tena mbele ya kiti kile kulionekana kama bahari ya kioo, kulingaa sana kama kilauri. Kile kiti cha kifalme kilikuwa kimezungukwa pande zote na viumbe vine vya ajabu, vyenye kujaa macho mbele na nyuma.


Kisha nikaangalia tena, nikasikia sauti ya wamalaika wengi wenye kuzunguka kiti cha kifalme, na viumbe vya ajabu na wazee. Hesabu yao ilikuwa maelfu na maelfu na mamilioni na mamilioni.


Nao waliimba hivi kwa sauti kubwa: “Mwana-Kondoo aliyeuawa anastahili kupokea uwezo, utajiri, hekima na nguvu, heshima, utukufu na sifa!”


Kisha nikaona mambo haya: Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa kwanza kati ya ile mihuri saba, nikasikia kimoja kati ya vile viumbe vya ajabu kikisema hivi kwa sauti kama ya ngurumo ya radi: “Kuja!”


Wakaaji wote wa dunia watamwabudu, ndio wale wote ambao tangia kuumbwa kwa dunia, majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite