Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 5:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Basi mumoja kati ya wale wazee akaniambia: “Usilie. Angalia, simba wa kabila la Yuda, wa uzao wa mufalme Daudi, amepata ushindi. Yeye anaweza kuvunja vile vifundo saba vya muhuri vya kizingo na kukifungua.”

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 5:5
25 Referans Kwoze  

Kutatokea chipukizi katika shina la Yese, tawi litachipuka toka mizizi yake.


“Mimi Yesu, nimemutuma malaika wangu kwa kuwashuhudia maneno haya yote katika kanisa. Mimi ni wa shina na wa uzao wa mufalme Daudi. Mimi ni nyota ya asubui.”


Kwa maana inajulikana wazi kwamba Bwana wetu alitoka katika kabila la Yuda, na juu ya kabila lile Musa hakusema hata neno moja linaloelekea ukuhani.


Isaya naye anasema: “Muzao wa Yese atatokea, atatawala watu wa mataifa, nao watamutumainia.”


Habari hiyo inaelekea Mwana wake ndiye Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye alizaliwa kimwili katika uzao wa mufalme Daudi. Lakini kwa namna ya Roho Mutakatifu, alihakikishwa kwa uwezo kuwa yeye ni Mwana wa Mungu kwa njia ya kufufuka kwake.


Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka.


Kisha nikaona mambo haya: Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa kwanza kati ya ile mihuri saba, nikasikia kimoja kati ya vile viumbe vya ajabu kikisema hivi kwa sauti kama ya ngurumo ya radi: “Kuja!”


Na kiti kile kilikuwa kimezungukwa na viti vingine makumi mbili na vine vya kifalme na juu ya viti vile kulikuwa kumeikaa wazee makumi mbili na wane. Wale wazee walikuwa wamevaa nguo nyeupe na juu ya kichwa chao kulikuwa taji za zahabu.


Yawe anasema hivi: Acha kulia, panguza machozi yako, maana utapata malipo kwa kazi yako. –Ni ujumbe wa Yawe.– Watoto wenu watarudi kutoka inchi ya waadui zenu.


Halafu mumoja wa wale wazee akaniuliza: “Wale wanaovaa kanzu nyeupe ni watu gani nao wanatoka wapi?”


wale wazee makumi mbili na wane waliinama uso mpaka chini mbele ya yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakimwabudu huyo anayeishi kwa milele na milele. Nao walikuwa wakikuja kuweka taji zao mbele ya kiti chake, na kusema:


Hizi ni habari za mambo yaliyofunuliwa na Yesu Kristo. Kristo alipata ufunuo huu kutoka kwa Mungu, kusudi awaonyeshe watumishi wake mambo yanayopaswa kutokea kisha kidogo. Kristo alimutuma malaika wake kwa kumujulisha mutumishi wake Yoane mambo yale.


Wale wamalaika wakamwuliza: “Ee mama, kwa sababu gani unalia?” Naye akawajibu: “Kwa sababu wameondoa maiti ya Bwana, nami sijui pahali walipoiweka.”


Bwana alipomwona yule mama, akamusikilia huruma na kumwambia: “Usilie.”


Atavizia na kulala chini kama simba, nani atasubutu kumwamusha? Abarikiwe yeyote atakayekubariki wewe Israeli, alaaniwe yeyote atakayekulaani.


Yesu akawageukia na kuwaambia: “Ninyi wanawake wa Yerusalema, musinililie mimi, lakini mujililie ninyi wenyewe pamoja na watoto wenu.


Watu wote walikuwa wakilia na kusikitika sana kwa ajili ya kifo cha mutoto. Lakini Yesu akasema: “Musilie, kwa maana hakufi, lakini analala tu!”


Nikajongea karibu na mutu mumoja kati ya wale waliosimama pale na kumwuliza maana kamili ya mambo hayo yote. Naye akanielezea maana yake akisema:


Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.


Nami nikalia sana, kwa sababu hakukuonekana mutu aliyestahili kufungua kizingo wala kuangalia ndani yake.


Kulikuwa vilevile sanamu kumi na mbili za simba wamesimama, mumoja kwa mwisho wa kila ngazi. Kiti kama hicho kilikuwa bado hakijatengenezwa katika ufalme wowote.


Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na kiti cha kuegemea miguu cha zahabu, vyote hivyo vilikuwa vimeshikamanishwa na kiti hicho cha kifalme; na kila upande kilikuwa na pahali pa kuegemeza mikono tena kilikuwa na sanamu mbili za simba karibu na pahali pale pa kuegemeza mikono.


Mishipa yake imeshikamana pamoja, imara kama chuma wala haitikisiki.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite