Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 4:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 wale wazee makumi mbili na wane waliinama uso mpaka chini mbele ya yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakimwabudu huyo anayeishi kwa milele na milele. Nao walikuwa wakikuja kuweka taji zao mbele ya kiti chake, na kusema:

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 4:10
28 Referans Kwoze  

Wakati alipokuwa amekwisha kukamata kizingo, vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee makumi mbili na wane wakainama uso mpaka chini mbele ya Mwana-Kondoo. Kila mumoja wao alikuwa na kinubi na vikombe vya zahabu vilivyojaa marasi, ndiyo maombi ya watu wa Mungu.


Na wale wazee makumi mbili na wane na vile viumbe vine vya ajabu wakainama chini na kumwabudu Mungu, anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakisema: “Amina! Mungu asifiwe!”


Na wale wazee makumi mbili na wane wanaokaa juu ya viti vyao vya kifalme mbele ya Mungu, wakainama uso mpaka chini wakimwabudu Mungu,


Mukuje tuiname chini na kumwabudu; tumupigie magoti Yawe, Muumba wetu!


Na kiti kile kilikuwa kimezungukwa na viti vingine makumi mbili na vine vya kifalme na juu ya viti vile kulikuwa kumeikaa wazee makumi mbili na wane. Wale wazee walikuwa wamevaa nguo nyeupe na juu ya kichwa chao kulikuwa taji za zahabu.


Na wamalaika wote waliokuwa wakizunguka kile kiti cha kifalme, wazee na vile viumbe vine vya ajabu, wakainama uso mpaka chini mbele ya kiti cha kifalme, nao wakamwabudu Mungu,


Vile viumbe vine vya ajabu vilijibu: “Amina.” Na wale wazee wakainama uso mpaka chini na kuabudu.


Ewe Bwana, hakuna asiyekuogopa, wala hakuna asiyekutukuza, kwa maana wewe peke yako ndiwe mutakatifu. Mataifa yote yatakuja kukuabudu, kwa maana matendo yako ya haki yameonyeshwa wazi.”


Wafalme wote wa dunia wamuheshimu, watu wa mataifa yote wamutumikie.


Vile viumbe vine vya ajabu viliimba kwa kumutukuza, kumuheshimia na kumushukuru yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme, yule anayeishi kwa milele na milele. Kila mara vilipofanya vile,


Kisha, mufalme Daudi akawaambia wote waliokusanyika: “Mumusifu Yawe, Mungu wenu.” Na wote waliokusanyika wakamutukuza Yawe, Mungu wa babu zao, wakainama mbele yake na kumwabudu Yawe na kumutolea mufalme Daudi heshima.


Wakaingia ndani ya nyumba, wakamwona mutoto pamoja na mama yake, Maria. Wakapiga magoti na kumwabudu mutoto. Kisha wakafungua mizigo yao na kumutolea zawadi ya zahabu, ubani na marasi.


Waisraeli wote walipoona moto ukishuka kutoka mbinguni na utukufu wa Yawe katika nyumba, wakainama nyuso zao zikifika mpaka chini. Wakamwabudu na kumushukuru Yawe wakisema: “Yeye ni muzuri. Wema wake unadumu milele.”


Nao walipokwisha kumwabudu, wakarudia Yerusalema wakifurahi sana.


Si sisi, ee Yawe, si sisi; lakini wewe peke yako utukuzwe, kwa ajili ya wema na uaminifu wako.


Kisha Yobu akasimama, akapasua nguo yake, akanyoa nywele zake, akajitupa chini na kumwabudu Mungu,


Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa sawa hivi ninavyokuwa, na neema yake niliyopewa haikukuwa ya bure, lakini nilitumika zaidi sana kuliko mitume wote wengine. Hakika si mimi, lakini ni neema ya Mungu inayokuwa pamoja nami.


Ninanyoosha mukono wangu mbinguni na kuapa: Kama vile ninavyoishi milele,


Mumwimbie Mungu mashairi ya sifa; maana yeye ni mufalme wa ulimwengu wote.


Katika mwaka mufalme Uzia alipokufa, nilimwona Bwana katika maono akiikaa katika kiti cha kifalme kinachoinuka juu sana. Pindo la nguo yake lilienea katika hekalu lote,


Na sasa, mimi Nebukadneza ninamusifu na kumutukuza na kumuheshimu Mufalme wa mbinguni. Maana matendo yake yote ni ya haki, naye anawashusha wenye kiburi.


Yule mutu aliyesimama upande wa juu wa muto, aliyevaa nguo za kitani, akainua mikono yake yote miwili kuelekea mbinguni. Kisha nikamusikia akiapa kwa jina la yule anayeishi milele: Itakuwa muda wa nyakati tatu na nusu. Wakati mateso ya watu watakatifu yatakapokomeshwa, mambo haya yote yatakuwa yametimia.


Na mara moja nikashikwa na Roho wa Mungu. Nikaona kiti cha kifalme kimewekwa kule mbinguni na mutu mumoja alikuwa akiikaa juu ya kiti kile.


Akaapa kwa jina la Mungu anayeishi kwa milele na milele, muumba wa mbingu na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake, nayo dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, pamoja na bahari na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake, na kusema: “Hakutakuwa tena muda unaobaki!”


Na mumoja wa vile viumbe vine vya ajabu akawapa wale wamalaika saba vikombe saba vya zahabu vyenye kujaa kasirani ya Mungu, anayeishi kwa milele.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite