Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 3:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Ninakuja upesi. Shika sana kile unachokuwa nacho, kusudi mutu yeyote asinyanganye taji yako ya ushindi.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 3:11
19 Referans Kwoze  

Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.


Yesu anasema: “Sikiliza, ninakuja upesi! Nitaleta mushahara kwa kulipa kila mumoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.


Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.


Lakini ninawaomba tu mushikamane na kile munachokuwa nacho mpaka nitakapokuja.


Tangia sasa nimetayarishiwa zawadi ya ushindi, ndiyo ile taji ya haki, ambayo Bwana anayekuwa Mwamuzi wa haki atakayonipa siku ile ya kurudi kwake. Wala hatanipa mimi peke yangu tu, lakini na wale wote wanaopenda kumwona wakati atakaporudi.


Vilevile mutu yeyote anayeshindana katika michezo hawezi kupata zawadi ya ushindi kama asipotii kanuni za michezo.


Mwenye kushuhudia maneno hayo anasema: “Ndiyo, ninakuja upesi!” Amina! Kuja Ee Bwana Yesu!


Heri yule anayesoma na wale wanaosikia maneno hayo ya unabii na kushika yale yaliyoandikwa ndani ya kitabu hiki, kwa maana wakati wa kutimia kwa mambo haya unakaribia.


wale wazee makumi mbili na wane waliinama uso mpaka chini mbele ya yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakimwabudu huyo anayeishi kwa milele na milele. Nao walikuwa wakikuja kuweka taji zao mbele ya kiti chake, na kusema:


Na kila mutu anayefanya mashindano katika michezo anajizuiza na vitu vingi katika mazoezi yake. Basi wanafanya hivi kusudi wapate taji yenye kuharibika; lakini sisi tunafanya vile, kusudi tupate taji isiyoharibika.


Basi ukumbuke mafundisho uliyopokea na yale uliyosikia. Uyashike na kugeuka toka zambi zako. Kama usipokesha, nitakuja kama mwizi, wala hautajua saa nitakapokuja kwako.


Na kiti kile kilikuwa kimezungukwa na viti vingine makumi mbili na vine vya kifalme na juu ya viti vile kulikuwa kumeikaa wazee makumi mbili na wane. Wale wazee walikuwa wamevaa nguo nyeupe na juu ya kichwa chao kulikuwa taji za zahabu.


Ninajua pahali pale unapokaa, ile ndiyo nafasi ya utawala wa Shetani. Wewe unashikamana na jina langu, wala haukuikana imani unayokuwa nayo kwangu, hata wakati Antipa, mushuhuda wangu mwaminifu, alipouawa kati yenu kule kwenye makao ya Shetani.


Yesu anasema: “Sikiliza, ninakuja upesi! Heri yule anayeshika maneno ya unabii yanayoandikwa katika kitabu hiki!”


Ile siku kubwa ya Yawe imekaribia, iko karibu na inakuja mbio. Mulio wa siku ya Yawe ni wa uchungu; hapo, hata shujaa atalia kwa sauti.


Wandugu zangu, musinungunikiane ninyi kwa ninyi kusudi Mungu asiwahukumu. Muangalie, mwamuzi ni karibu, naye amekuwa kwenye mulango!


Muonyeshe upole wenu kwa watu wote, kwa maana Bwana yuko karibu kurudia.


“Sikiliza, ninakuja kwa saa isiyozaniwa kama vile mwizi. Heri yule anayekesha na kutunza nguo zake vizuri kusudi asitembee uchi na kujifezehesha mbele ya watu.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite