Ufunuo 22:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Kisha yule malaika akanionyesha muto wa maji ya uzima wenye kungaa kama kioo, uliokuwa ukitiririka toka kwenye kiti cha kifalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo.
Kwa maana Mwana-Kondoo anayekuwa katikati ya kiti cha kifalme, atawachunga na kuwaongoza kwenye chemichemi ya maji ya uzima. Naye Mungu atawapanguza machozi yao yote.”
lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”
Akasema tena: “Sasa ni mwisho! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Yule anayesikia kiu, nitamupa maji ya kunywa yanayotoka katika chemichemi ya maji ya uzima pasipo kulipa.
Wakati ule, maji ya uzima yatabubujika kutoka Yerusalema, na nusu ya maji yale yatatiririkia kwenye bahari ya mashariki, na nusu ingine kwenye bahari ya magaribi. Maji yale yataendelea kububujika wakati wa kipwa kama yanavyokuwa wakati wa mvua.
Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.
Ee Yawe, tumaini la Waisraeli, wote wanaokukataa wafezeheshwe. Wanaokuacha wewe watatoweka, kama majina yaliyoandikwa chini katika mavumbi, kwa maana wamekuacha wewe Yawe, unayekuwa chemichemi ya maji ya uzima.
Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.
Na kisha kunyanyuliwa aikae na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Baba yake, yeye akamupa Roho Mutakatifu aliyeahidiwa. Naye akamushusha juu yetu, sawa vile munavyojionea na kusikia wenyewe.
Nikasikia vilevile viumbe vyote vinavyokuwa mbinguni, katika dunia, katika kuzimu na vile vinavyokuwa katika bahari; viumbe vyote vya ulimwengu nzima vikimwimbia: “Utukufu, heshima, sifa na nguvu milele na milele, kwa yule anayeikaa juu kiti cha kifalme na kwa Mwana-Kondoo.”
Halafu nikaona Mwana-Kondoo akisimama katikati ya kiti cha kifalme chenye kuzungukwa na vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee, naye alionekana kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba; ndizo roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote.
Maana Yawe anasema hivi: Nitakuletea fanaka nyingi kama muto, utajiri wa mataifa kama muto uliofurika. Nanyi mutanyonya na kubebwa kama mutoto muchanga, mutabembelezwa kama mutoto juu ya magoti ya mama yake.
Hizi ni habari za mambo yaliyofunuliwa na Yesu Kristo. Kristo alipata ufunuo huu kutoka kwa Mungu, kusudi awaonyeshe watumishi wake mambo yanayopaswa kutokea kisha kidogo. Kristo alimutuma malaika wake kwa kumujulisha mutumishi wake Yoane mambo yale.
Kisha mumoja wa wale wamalaika saba walioshika vile vikombe vilivyojaa mapigo saba ya mwisho, akajongea na kuniambia: “Kuja nitakuonyesha bibi arusi, muke wa Mwana-Kondoo.”
Kisha yule malaika akaniambia: “Maneno haya ni ya kweli na ya uhakika. Na Bwana Mungu anayewaongoza manabii kwa njia ya Roho wake ametuma malaika wake kwa kuwaonyesha watumishi wake mambo yanayopaswa kutokea kisha kidogo.”