Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 21:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 21:3
29 Referans Kwoze  

Nitaishi kati yao; nitakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wangu.


Kuna ulinganisho gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi ni hekalu la Mungu Mwenye Uzima kama vile yeye mwenyewe alivyosema: “Nitakaa na kuishi pamoja nao, nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”


Yesu akamujibu: “Anayenipenda, atashika maneno yangu. Baba yangu atamupenda, naye Baba pamoja nami tutaingia ndani yake na kukaa ndani yake.


na kuwafanya wakae katika Yerusalema. Wao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; nitatawala juu yao kwa uaminifu na haki.


Sasa hili ndilo agano nitakalofanya na watu wa ufalme wa Israeli katika siku zile: nitawawezesha kuchunga sheria zangu ndani ya mafikiri yao, nikiziandika ndani ya mioyo yao. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.


Kisha siku hizo, nitafanya agano hili na Waisraeli. Nitaiweka sheria yangu ndani yao, na kuiandika katika mioyo yao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Lakini kwa hakika walitamani sana inchi inayokuwa bora zaidi, ndiyo inchi ya mbinguni. Kwa sababu hii Mungu hasikii haya kuitwa Mungu wao, maana amewatayarishia muji.


Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.


Nao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.


Ndiyo maana wanasimama mbele ya kiti cha kifalme cha Mungu, nao wanamutumikia muchana na usiku katika hekalu lake. Na yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme atawalinda katika hema yake.


Nitakuwa Baba yenu nanyi mutakuwa wana na wabinti wangu. Ni mimi Bwana Mwenye Uwezo ninayesema.”


Yule atakayeshinda atapokea toka kwangu zawadi ile, mimi nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwana wangu.


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.


Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni, ikisema: “Sasa wokovu, uwezo na ufalme wa Mungu, na mamlaka ya Kristo wake vimefika. Ni vile, kwa yule aliyekuwa akiwashitaki wandugu zetu mbele ya Mungu wetu muchana na usiku ametupwa chini ya mbingu.


naye akaniambia: Wewe mwanadamu! Hapa ndipo pahali pa kiti changu cha kifalme, pahali ninapoweka miguu yangu. Nitakaa kati ya watu wa Israeli milele. Na Waisraeli hawatalichafua jina langu, wao wenyewe, wala wafalme wao kwa kuziabudu sanamu au kuzika maiti za wafalme wao pahali hapa.


“Lakini, ee Mungu, kweli utakaa katika dunia? Ikiwa hata mbingu zenyewe wala mbingu za juu sana hazikutosha, namna gani nyumba hii ambayo nimeijenga itakutoshelea?


“Lakini, ee Mungu kweli utakaa humu katika dunia na wanadamu, ikiwa hata mbingu zenyewe, wala mbingu za mbingu za juu sana hazikutoshi? Namna gani nyumba hii ambayo nimejenga itakutoshelea?


Kisha nikasikia tena sauti kutoka mbinguni ikiniambia: “Kwenda utwae kile kitabu kidogo chenye kufunguliwa katika mukono wa yule malaika anayesimama juu ya bahari na juu ya inchi kavu.”


Na ngurumo zile saba zilipokwisha kusikilika, nikajitayarisha kwa kuandika. Lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni, ikiniambia hivi: “Uchunge kwa siri maneno yaliyosemwa na zile ngurumo saba.”


Vilevile Waisraeli watanitengenezea hema takatifu, kusudi niweze kukaa kati yao.


Nitaishi kati ya Waisraeli, nami nitakuwa Mungu wao.


Jumla ya urefu wa kuta zote ine utakuwa ni metre elfu kenda. Jina la muji kutokea sasa na kuendelea litakuwa: Yawe Yupo Hapa.


Basi Mungu mwenyewe, Baba yetu, na Bwana wetu Yesu, watufungulie njia tupate kufika kwenu.


Yeye anafanya kazi ya Kuhani Mukubwa katika Pahali Patakatifu Sana, maana yake katika hema ya kweli iliyosimikwa na Bwana, wala si mutu.


Hakutakuwa tena kitu chochote kinacholaaniwa na Mungu. Kiti cha kifalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwa ndani ya muji ule, na watumishi wa Mungu watamwabudu.


Hivi ndivyo ilivyokuwa kila siku; wingu lilifunika hema muchana, na usiku lilionekana kama moto.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite