Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 21:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Ulikuwa ukizungukwa na ukuta mukubwa na murefu wenye milango kumi na miwili na wamalaika kumi na wawili walichunga milango ile. Na juu ya milango ile, kulikuwa kumeandikwa majina ya makabila kumi na mawili ya Waisraeli.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 21:12
21 Referans Kwoze  

Milango ya muji ule haitafungwa muchana maana ndani yake hakutakuwa usiku.


Minara yako nitaijenga kwa mawe ya akiki, milango yako kwa almasi, na ukuta wako kwa mawe ya bei kali.


Ndani ya kuta zinazokuzunguka kuwe amani, nao usalama ukuwe ndani ya nyumba zako nzuri!”


Mateso makali hayatasikilika tena katika inchi yako; wala uharibifu na maangamizi ndani ya mipaka yako. Utaweza kuziita kuta zako: “Wokovu”, na milango yako: “Sifa”.


Kweli wewe haupendezwi na sadaka. Hautaki nikutolee sadaka za kuteketezwa.


Kisha wakati wa kuzindua ukuta wa Yerusalema Walawi wakatafutwa kila pahali walipokaa kwa kuja Yerusalema kusherehekea kwa furaha pamoja na shukrani na nyimbo, wakitumia matoazi, vinubi na zeze.


Makabila yetu kumi na mawili wanamwabudu Mungu usiku na muchana, kwa maana wanatumaini kuona utimilifu wa ile ahadi. Na ni kwa sababu ya tumaini lile, Ee mufalme, Wayuda wananishitaki.


Haukutuacha tuishi katika utumwa ingawa tulikuwa watumwa. Uliwafanya wafalme wa Persia wakuwe wema kwetu na kuturuhusu tuishi na kuijenga nyumba yako iliyokuwa imebomoka, na ukatufanya tukae salama hapa Yuda na Yerusalema.


Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.


Siku moja yule masikini akakufa, na wamalaika wakamupeleka mpaka pembeni ya Abrahamu. Na yule tajiri akakufa vilevile na kuzikwa.


Vilevile ninawaambia, ndivyo wamalaika wa Mungu wanavyofurahi kwa ajili ya mwenye zambi mumoja anayegeuka toka zambi zake.”


“Mufanye angalisho, musimuzarau mumoja wa hawa wadogo; kwa sababu ninawaambia kwamba wamalaika wao wanaokuwa mbinguni wako siku zote karibu na Baba yangu anayekuwa mbinguni. [


Basi, kutakuwa mawe kumi na mawili yaliyochorwa majina kumi na mawili ya wana wa Israeli. Kila moja litakuwa kama muhuri, kwa kusimamia makabila yale kumi na mawili.


Kila upande kulikuwa milango mitatu: upande wa mashariki milango mitatu, upande wa kaskazini milango mitatu, upande kusini milango mitatu na upande wa magaribi milango mitatu.


Malaika yule aliyekuwa akisema nami alikuwa na fimbo ya kupima ya zahabu kusudi apate kupima muji ule, milango yake na ukuta unaouzunguka.


Heri wale wanaosafisha kanzu zao, kwa maana watakuwa na haki ya kukula matunda ya muti wa uzima na ya kuingia katika muji ule kwa kupitia kwenye milango.


Palikuwa sanamu kumi na mbili za simba waliosimama kwa mwisho wa kila ngazi. Kiti kama hicho kilikuwa bado kutengenezwa katika ufalme wowote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite