Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 21:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 nao ukingaa kwa utukufu wa Mungu. Mwangaza wake ulikuwa kama jiwe la bei kali la yaspi, linalongaa kama kioo.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 21:11
17 Referans Kwoze  

Hakutakuwa usiku tena, wala hawatakuwa na lazima ya mwangaza wa taa wala jua, kwa sababu Bwana wetu na Mungu wetu mwenyewe atawaangazia, nao watatawala milele na milele.


Tena mbele ya kiti kile kulionekana kama bahari ya kioo, kulingaa sana kama kilauri. Kile kiti cha kifalme kilikuwa kimezungukwa pande zote na viumbe vine vya ajabu, vyenye kujaa macho mbele na nyuma.


Kisha yule malaika akanionyesha muto wa maji ya uzima wenye kungaa kama kioo, uliokuwa ukitiririka toka kwenye kiti cha kifalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo.


Juu ya vichwa vya vile viumbe kulikuwa kitu kinachofanana na anga, kinangaa kama kioo.


Mutu yule aliangaa kama mawe ya bei kali ya yaspi na sardio. Kiti kile cha kifalme kilikuwa kimezungukwa na upindi wa mvua uliongaa kama jiwe la zumaridi.


Jumla ya urefu wa kuta zote ine utakuwa ni metre elfu kenda. Jina la muji kutokea sasa na kuendelea litakuwa: Yawe Yupo Hapa.


Juu ya kitu hicho niliona kitu kimoja kinachofanana na kiti cha kifalme chenye rangi la jiwe la yakuti. Juu yake kulikuwa kunaikaa kitu kinachofanana na mutu.


Halafu, kila pahali juu ya mulima Sayuni na juu ya mikutano ya watu atafanya kuwe wingu wakati wa muchana, na moshi na moto unaowaka vizuri wakati wa usiku. Zaidi ya hayo utukufu wa Mungu utaufunika na kuulinda muji wote.


Zahabu au kioo havilingani nayo, wala haiwezi kubadilishwa na mawe ya zahabu safi.


Hekalu likajaa moshi kutokana na utukufu wa Mungu na uwezo wake. Na hakuna mutu aliyeweza kuingia ndani ya hekalu mpaka yale mapigo yaliyoletwa na wale wamalaika saba yalipotimizwa.


Utukufu wa Mungu wa Israeli ulitokea upande wa mashariki. Pamoja nao kulikuwa mushindo wa kuja kwake kama mushindo wa maji mengi, inchi ilingaa kwa utukufu wake.


Ustawi wa biashara yako ulikujaza ukali, ukatenda zambi. Kwa hiyo nilikufukuza kama muchafu, mbali na mulima wangu mutakatifu. Na yule kerubi aliyekulinda akakufukuzia mbali na mawe yanayometameta.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite