Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ufunuo 2:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 “Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoambia makanisa! “Yule atakayeshinda hatapatwa na kifo cha pili.

Gade chapit la Kopi




Ufunuo 2:11
16 Referans Kwoze  

Heri na baraka sana kwa wale watakaokuwa katika ufufuko wa kwanza! Kifo cha pili hakina uwezo juu yao, nao watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, na watatawala pamoja naye kwa muda wa miaka elfu moja.


Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.”


Kisha kifo na kuzimu vikatupwa katika ziwa la moto. Ziwa lile la moto ndicho kifo cha pili.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda nitamupa ruhusa ya kula matunda ya muti wa uzima unaokuwa katika bustani ya Mungu!


“Mwenye kuwa na masikio, asikie.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda, nitamupa ile mana iliyofichwa. Na nitamupa vilevile jiwe dogo jeupe, na juu yake kumeandikwa jina jipya ambalo hakuna mutu yeyote anayelijua, isipokuwa tu yule anayelipewa.


Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!


Basi mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!”


Kisha akawaambia: “Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!”


Lakini mbegu zingine zikaanguka katika udongo muzuri; nazo zikaota na kutoa matunda, kila moja punje mia.” Yesu alipokwisha kuwaambia hayo yote, akasema: “Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!”


Yule atakayeshinda atavalishwa nguo nyeupe, nami sitafuta jina lake kati ya majina yanayoandikwa katika kitabu cha uzima. Nami nitamutetea mbele ya Baba yangu na mbele ya wamalaika zake.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa!


Yule atakayeshinda nitamufanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, naye hatatoka tena mule. Na zaidi ya ile nitaandika juu yake jina la Mungu wangu na jina la muji wa Mungu wangu, ndio Yerusalema mupya, utakaoshuka toka mbinguni kwa Mungu wangu. Nitaandika vilevile juu yake jina langu jipya.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa.


Yule atakayeshinda atapokea toka kwangu zawadi ile, mimi nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwana wangu.


Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie.]”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite